KAMANDA wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, ACP Jumanne Muliro, amesema watu sita kati ya tisa wanaotuhumiwa kwa ujambazi, wamejeruhiwa na risasi wakati wakijibizana na Polisi walipovamia kiwanda kimoja jijini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Kamanda Muliro ametoa taarifa hiyo leo Ijumaa, tarehe 22 Julai 2022, alipotembelea kiwanda hicho kilichopo maeneo ya Keko, Dar es Salaam, baada ya kuvamiwa na watuhumiwa hao usiku wa kuamkia leo.
Amesema majeruhi hao wamefikishwa hospitalini kwa ajili ya matibabu, huku watatu waliobakia wakiendelea kuwa mikononi mwa polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi.
“Jeshi likapata taarifa kwa hiyo Polisi wakaja haraka eneo la tukio wakalikuta kundi hilo la wahalifu ambao majambazi, wakaanza kuwatihsia na kushambulia mmoja alikuwa na silaha, askari wakajihami kwa silaha baadae wakasalimu amri,” amesema Kamanda Muliro na kuendelea:
“Majambazi wapatao sita walijeruhiwa kwenye miili yao na wamepelekwa haraka hospitali kwa matibabu ili tuweze kupata fursa za kuwahoji kwa kina. Wengine tuko nao na uchunguzi wa tukio unaendelea na mali walizotaka kuiba zaidi ya maboksi 70 zimeokolewa.”
Leave a comment