Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Shule, vyuo kuendelea kufungwa, Rais Magufuli afuta sherehe za Muungano
AfyaHabari za SiasaTangulizi

Shule, vyuo kuendelea kufungwa, Rais Magufuli afuta sherehe za Muungano

Spread the love

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema agizo la kufungwa kwa shule na vyuo vya kati na vya elimu ya juu, liliotolewa tarehe 17 na 18 Machi mwaka huu, litaendelea  hadi pale serikali itakapotoa taarifa nyingine. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Waziri Mkuu amesema wamefikia maamuzi hayo kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa wa Homa Kali ya Mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19), kutoka 49 hadi kufikia 53.

Kufuatia ongezeko hilo, Waziri Majaliwa amesema pia, Rais John Magufuli amesitisha maadhimisho ya miaka 56 ya  Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, pamoja na Siku Kuu ya Wafanyakazi (Mei Mosi).

Taarifa hizo zimetolewa leo tarehe 14 Aprili 2020 jijini Dodoma, na Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu, wakati akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Kuratibu mapambano dhidi ya COVID-19.

Waziri Majaliwa amesema, Rais Magufuli ameagiza kiasi cha Sh. 500 milioni zilizopangwa kufanyia sherehe za maadhimisho ya muungano, zipelekwe katika Mfuko wa Kupambana na ugonjwa huo, wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Amesema sherehe hizo zimesitishwa ili kuzuia mikusanyiko, inayoweza sababisha kuenea kwa ugonjwa huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!