Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sheikh Ponda ataka mwarobaini changamoto uchaguzi 2020
Habari za Siasa

Sheikh Ponda ataka mwarobaini changamoto uchaguzi 2020

Sheikh Ponda Issa Ponda (katikati)
Spread the love

KATIBU Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, amesema changamoto zilizojitokeza katika Uchaguzi Mkuu wa 2020, kama hazitajadiliwa kwa uzito na kutafutiwa mwarobaini, huenda zikatijitokeza katika chaguzi zijazo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Sheikh Ponda ametoa kauli hiyo leo tarehe 30 Novemba 2023, akizungumza na MwanaHALISI kwa njia ya simu.

Kiongozi huyo wa kidini amedai kuwa, kinachoendelea sasa ni upande wa Serikali kutoa kauli za kutaka maridhiano kufuatia changamoto hizo zilizojitokeza ikiwemo madai ya baadhi ya wananchi kujeruhiwa, kupoteza maisha na wagombea kuenguliwa, bila ya kuchukua hatua za kutengeneza mazingira mazuri ili zisijirudie.

“Ukweli ni kwamba, kama yale madhila yaliyotokea 2020 yanazungumzwa katika lugha kama vile ya kupuuza, sababu watu wanaoonesha hisisa zao kuhusu matatizo yaliyokuwepo kwenye uchaguzi, wanasema tusameheane tusitonesehe vidonda,” amesema Sheikh Ponda.

Sheikh Ponda amesema “lakini kuna watu wameuawa hapakuwa na jambo la kuchukuliwa hatua zozote zile, walioathirika hawajalipwa fidia. Serikali haijaweka mikakati ya pamoja kuhakikisha hili halitatokea tena kwenye uchaguzi, badala yake inasema tusameheane.”

Wakati Sheikh Ponda akitoa kauli hiyo, Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, imechukua hatua mbalimbali kukutana na vyama vya siasa hususan vya upinzani, ili kutafuta maridhiano kwa lengo la kutafuta suluhu ya madhila yaliyojitokeza katika demokrasia hususan wakati wa uchaguzi.

Tayari Serikali imewasilisha bungeni jijini Dodoma, marekebisho ya sheria za uchaguzi, ili kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na wadau kwa ajili ya kuboresha mazingira ya chaguzi zijazo.

“Kama hayatajadiliwa kwa uzito unaotakiwa, matokeo yake tutaingia kwenye uchaguzi katika hali hiyo. Ili kusaidia tatizo kupungua inabidi yawekewe kipaumbele,” amesema Sheikh Ponda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!