Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali ya Tanzania yamwita kumhoji Balozi wa Marekani
Habari za Siasa

Serikali ya Tanzania yamwita kumhoji Balozi wa Marekani

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania, imemwita Kaimu Balozi wa Marekani nchini humo, Dk. Imni Patterson ili kumhoji juu ya masuala mbalimbali ambayo ubalozi huo umekuwa ukiyaandika katika mitandao yake ya kijamii bila ya uthibitisho ikiwemo ugonjwa wa COVID-19. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa iliyotolewa leo Jumanne tarehe 26 Mei 2020 na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Tanzania, Emmanuel Buhohela imesema, mazungumzo kati ya Balozi Imni na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Kanali Wilbert Ibuge yamefanyikia ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.

Buholela amesema, katika mazungumzo hayo, Kanali Ibuge ameonyesha masikitiko yake juu ya taarifa ambazo Marekani imekuwa ikizitoa kuhusu usafiri kwa raia wake.

Katika taarifa hiyo, inasema, Kanali Ibuge ametolea mfano wa taarifa zilizotolewa na Marekani katika mtandao wa Twitter tarehe 13 na 25 Mei, 2020 kwa raia wake ukielezea hali ya corona jijini Dar es Salaam si nzuri.

Kanali Ibuge amesema, taarifa hizo zinaelezea jinsi hospitali za jiji la Dar es Salaam vilivyosheheni wagonjwa wa corona ilihali si kweli jambo, jambo linaloweza kuleta taharuki kwa Watanzania na raia wengine wa kigeni kutoka mataifa mbalimbali.

Katibu mkuu huyo, amemtaka Balozi Imni kutoa taarifa zilizothibitishwa kwani Tanzania haina kizuizi chochote kwa mabalozi wanaohitaji taarifa hizo.

Katika mazungumzo hayo, Kanali Ibunge ametumia fursa hiyo kumshukuru Balozi hiyo kwa ushirikiano anaoutoa na kuendeleza ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Marekani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!