Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali wawatunishia misuli wanunuzi wa korosho
Habari za Siasa

Serikali wawatunishia misuli wanunuzi wa korosho

Spread the love

SERIKALI imetoa siku nne kwa wanunuzi takribani 35 waliojitokeza kununua korosho, kupeleka barua katika Ofisi ya Waziri Mkuu inayoonesha kiasi cha tani wanazohitaji na siku watakazozichukua. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 9 Novemba 2018 jijini Dodoma na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati akitoa tamko la serikali kuhusu ununuzi wa zao la korosho.

Majaliwa ameeleza kuwa, siku hizo zikipita bila ya wanunuzi hao kutekeleza agizo hilo, serikali italazimika kufuta usajili kwa wote waliojisajili kununua zao hilo.

“Mwenye nia ahakikishe katika siku hizo nne iwe ndio mwisho wa kununua korosho, na waandike barua kwani ofisi yangu ipo wazi saa 24 wana nafasi ya kuleta barua wakati wowote wakionesha nia yao na kiwango wanachokihitaji, zaidi ya hapo serikali haitoruhusu kampuni yoyote kununua korosho tena,” amesema Majaliwa.

Majliwa amesema wakati Rais John Magufuli alipozungumza na wanunuzi wa korosho walikubaliana kununua zao hilo kwa bei inayoanzia Sh. 3,000 na kuendelea, na kwamba baada ya kikao hicho ununuzi katika minada imeendelea kusuasua na tani zilizonunuliwa zilikuwa kidogo sana.

Amesema hali hiyo ni kama mgomo baridi kitendo ambacho si sawa kwani malengo ya serikali na sekta binafsi ni kumfanya mkulima apate bei nzuri.

“Hali hii haifurahishi kwa sababu serikali imedhamiria kuboresha mazao yanayolimwa na wakulima kwa kuwasaidia kuanzia katika hatua za utayarishaji wa mashamba, upatikanaji wa pembejeo na masoko ili waweze kunufaika na kilimo na kupata tija katika mazao hayo,” amesema Majaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!