Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Samatta arudi tena Ubelgiji, aitosa Genk
Michezo

Samatta arudi tena Ubelgiji, aitosa Genk

Mbwana Samatta
Spread the love

 

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta amerejea tena katika Ligi kuu ya Ubelgiji baada ya jana tarehe 31 Agosti, 2021 kusajiliwa na klabu ya Royal Antwerp FC inayoshiriki ligi kuu nchini humo. Anaripoti Damas Ndelema, TUDARCo … (endelea).

Mshambuliaji huyo raia wa Tanzania amerudi Ubelgiji baada ya kupitia baadhi ya klabu ya Aston Villa ya Uingereza na Fenarbach ya Uturuki.

Samatta alishawahi kuitumikia KRC Genk ya Ubelgiji ambayo ilimuibua na kumfanya awike Ulaya kiasi cha kumpa faida ya kutua katika soka la England.

Mshambuliaji huyo baada ya kuondoka nchini Ubelgiji wengi walimtabiria mazuri lakini bahati haikuwa kwake katika sehemu alizopita hakupata nafasi ya kutosha kulinganisha na alipokua Ubelgiji katika klabu ya Genk.

Aidha, wengi walitarajia Samatta atarudi nyumbani katika klabu ya KRC Genk kama walivyofanya baadhi ya mastaa kurudi katika klabu zao za zamani.

Christiano Ronaldo amerejea Manchester united, Antonio Griezman amerejea Atletico madrid wakati Romelu Lukaku amerejea Chelsea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!