Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Salum Mwalimu ampigia kampeni Ado wa ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Salum Mwalimu ampigia kampeni Ado wa ACT-Wazalendo

Salum Mwalimu, Mgombea Mwenza wa Urais Tanzania kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

USHIRIKIANO kati ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na ACT-Wazalendo katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 28 Oktoba 2020 umeanza kushika kasi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Viongozi wa vyama hivyo katika nyakati tofauti, wametoa kauli za ushirikiano katika Uchaguzi wa Urais wa Tanzania na Zanzibar, ubunge na udiwani huku Chadema kikitoa kauli rasmi ya kumuunga mkono Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia wa ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad.

Jana Jumatano tarehe 7 Oktoba 2020, Mgombea mwenzas wa Rais kupitia Chadema, Salum Mwalimu alimnadi Mgombea Ubunge wa Tunduru Kaskazini mkoani Ruvuma, Ado Shaibu kupitia Chama cha ACT-Wazalendo.

Mwalimu alifanya tukio hilo katika mkutano wa kampeni wa uliofanyika jimboni humo.

“Kama ni Ado lazima tumhakikishie maslahi yake ya ushindi yanakuaje hatuwezi kumuacha, tutakwenda na Ado lakini kamanda wetu huyu tusimuache lazima tuweke akiba mbele ya safari huko,” alisema Mwalimu.

Mwalimu ambaye ni Naibu Katibu Mkuu Chadema Zanzibar, ameutaka uongozi wa Chadema na wafuasi wa chama hicho katika Jimbo la Tunduru Kaskazini kumuunga mkono Ado, kwa kuwa anaushawishi mkubwa kwa wananchi ikilinganishwa na mgombea wao.

“Mnajua nani tunayetamani atuongoze, kwenye vyama vyetu hivi kuna wagombea udiwani na ubunge ili vyama vyetu hivi yako maeneo ambayo tukicheza vibaya tunaipa nguvu CCM lakini tukicheza vizuri CCM anakosa, hawezi akashidna hata akiongeza kura za wizi,” amesema Mwalimu.

Jumapili ya tarehe 4 Oktoba 2020, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alitangaza kumuunga mkono Maalim Seif katika kinyang’anyiro cha Urais Zanzibar, huku akisema mgombea wao Said Issa Mohammed ameridhia kujitoa katika uchaguzi huo.

Ado Shaibu, Mombea Ubunge Tunduru kupitia ACT-Wazalendo

Hali kadhalika Maalim Seif, katika mkutano wake wa kampeni visiwani Zanzibar uliofanyika hivi karibuni alitangaza rasmi kumuunga mkono, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chadema, Tundu Lissu.

Vile vile, Lissu alipofanya mkutano wake wa kampeni mkoani Kigoma katika Jimbo la Kigoma Mjini, aliwataka wafuasi wa Chadema kumchagua mgombea mwenye nguvu katika jimbo hilo.

Zitto Kabwe, Mgombea Ubunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT-Wazalendo, anaonekana kuwa na ushawishi mkubwa katika uchaguzi wa jimbo hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!