Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Rita yataka wananchi kuandika mirathi, kutunza na kuhifadhi wosia
Tangulizi

Rita yataka wananchi kuandika mirathi, kutunza na kuhifadhi wosia

Meneja Masoko na Mawasiliano wa RITA, Josephat Kimario
Spread the love

 

WAKALA wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), umewataka wananchi kuchangamkia huduma zinazotolewa na taasisi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma leo Jumanne, Afisa Msajili wa RITA, Nyanda Masunda, amesema shirika lake, limejipanga kutoa huduma ya msaada wa kisheria juu masuala mbalimbali yanayosimamiwa na taasisi hiyo.

Rita – kwa mujibu wa sheria za Tanzania Bara – ndilo shirika lililoruhusiwa kusimamia mirathi, kutunza na kuhifadhi wosia, pamoja na kusajili vyeti vya kuzaliwa.

Ametoa kauli hiyo, kwa lengo la kuwahamisha wananchi waweze kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho ya siku ya maadili na  haki za binadamu  yanayofanyika katika viwanja vya Nyerere Square, mjini Dodoma.

“Muitikio wa watu bado ni mdogo, hivyo tunawasihi wananchi kujitokeza kwa wingi, kwani RITA ipo hapa na timu nzima ya wanasheria wetu kukupa ushauri wa kisheria juu ya mambo ya mirathi na namna bora ya kuandika wosia na kutunza kumbukumbu,” ameeleza Nyanda.

Aliongeza: “Hii ni fursa kubwa kwa wakazi wa  Dodoma na maeneo ya jirani.”

Nyanda amesema,  RITA inaendelea kusogea karibu na wananchi ili kuwapa elimu ya wosia na mirathi, lengo ni kupunguza  migogoro mbalimbali ya kifamilia na mashauri ya mirathi kwenye mahakama zetu.

Maadhimisho ya siku ya haki za binadamu kitaifa, hufanyika  kila  tarehe 10 Desemba ya kila mwaka, ambapo mwaka huu kauli mbiu yake ni “Maadili, Hakiza Binadamu, Utawala Bora na Mapambano dhidi ya Rushwa, ni jukumu la pamoja kati ya serikali na  wadau wengine.

RITA kama wadau wapo kwa ajili ya kutoa huduma kadhaa, ambazo ni kikwazo katika mapambano katika utetezi wa haki za binadamu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!