Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Chalamila ‘akomalia’ daladala Mbeya
Habari za Siasa

RC Chalamila ‘akomalia’ daladala Mbeya

Spread the love

 

ALBER Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya amesema, serikali haitaondoa bajaji wala pikipiki (bodaboda), kufanya biashara ya kusafirisha abiria katika barabara kuu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya…(endelea).

Ametoa kauli hiyo leo Jumatatu tarehe 15 Machi 2021, baada ya asubuhi ya leo, kutokea mgomo wa daladala wakitaka bajaji na bodaboda kupigwa marufuku kusafirisha abiria kupitia barabara kuu ya Uyole- Mbalizi na Uyole- Soko Matola

“Hatuziondoi Bajaji ,” amesema Chalamila akisisitiza kwamba, endapo daladala zitaendelea kugoma, basi ataagiza mabasi ya serikali ikiwa ni pamoja na magereza, polisi na mahakama kubeba abiria hasa wanafunzi.

Chalamila amasema, bajaji na pikipiki wataendelea kutumia barabara hiyo, kwa sababu ni haki yao na wanalipa kodi kama wengine.

Kwenye vituo vya daladala cha Kabwe, Mbeya leo kulikuwa na idadi kubwa ya abiria baada ya daladala kugoma.

Daladala walichukua hatua hiyo kwa madai, bajaji na pikipiki zinavuruga biashara hiyo na hivyo kushinikiza kuondolewa barabara kuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!