Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko RC achamaa maafisa kilimo kitotembelea wakulima
Habari Mchanganyiko

RC achamaa maafisa kilimo kitotembelea wakulima

Mkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael
Spread the love

MKUU wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael amewapa onyo maafisa kilimo wa wilaya zote mkoani humo kuacha kukaa maofisini na badala yake waende vijijini kuwapa ushauri wa kitaalam wakulima. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe … (endelea).

Dk. Michael aliyasema hayo leo tare he 14 Novemba, 2023 wakati wa kikao cha wadau wa kilimo kilichofanyika kwenye ukumbi ulipo kwenye ofisi za mkoa huo.

Alisema yeye kama mkuu wa mkoa amekuwa akifanya ziara za kikazi vijijini kila wakati huku akiwashangaa maafisa hao kukaa maofisini licha ya serikali kuwapa  pikipiki na mafunzo ya mara kwa mara.

“Mmepewa usafiri wa pikipiki na Rais Dk. Samia muwatembelee wakulima lakini ninyi hamfanyi hivyo, mnakwenda nazo kwenye mabaa, katibu tawala shughurika na watumishi hawa waende vijijini.” amesema Dk. Michael.

Ameongeza kuwa vijiiini wakulima wengine hawajuhi mbolea watazipataje, badala wapate ufafanuzi na msaada kwa maafisa kilimo lakini hawaonekani kwa wakulima, na kwamba anapokuwa vijijini anazipata taarifa zote.

Katibu tawala mkoani Songwe Happiness Seneda aliyapokea magizo hayo huku akiruhusu wadau wa kilimo kutoa changamoto zinazohusu kilimo ambapo malalakiko yaliyotolewa ni maafisa hao kutofika vijijini na kupanda bei ya mbegu za mahindi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!