Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Msiogope mabadiliko, hakuna atakayepoteza ajira
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia: Msiogope mabadiliko, hakuna atakayepoteza ajira

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amewatoa hofu waajiriwa katika taasisi na mashirika ya umma yatakayofutwa kutokana na sababu mbalimbali kwamba watahamishiwa kwenye mashirika mengine kwani Serikali haiwezi kupoteza nguvu kazi yao. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya Ofisi ya msajili wa hazina kufanya uchambuzi na kubaini taasisi ambazo majukumu yanashabihiana na nyingine ambazo kwa sasa majukumu yake yamepitwa na wakati huku nyingine utendaji wake unalegalega.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Agosti 2023 wakati akifungua kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wa mashirika ya umma kinachofanyika jijini Arusha.

“Katika maboresho tunayoyafanya hakuna nguvukazi au ajira itakayopotea, wote ambao wapo kwenye mshirika aidha watamezwa kwingine au kutakuja mashirika mengine yenye maana sasa kuliko wakati yalipoanzishwa. Naomba msihofu msiogope mabadiliko yaliyopo,” amesema.

Amesema Serikali inafanya hivyo kwa sababu, takwimu zinaonesha asilimia 17 ya ajira nchini inatolewa na taasisi, mashirika na wakala hivyo haiwezi kuyaondoa ili ajira zipotee.

Amesema mpango huo utaipunguzia serikali gharama za uendeshaji na kuongezea ufanisi.

“Tumeambiwa mashirika haya ndio nguzo kuu ya maendeleo ya serikali, nguzo ya uchumi wa serikali. Yakizalisha wa vizuri Serikali inapata tija na kufanya makubwa zaidi, yakiwa mzigo inarudisha nyuma maendeleo ya serikali,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!