Saturday , 30 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Msiogope mabadiliko, hakuna atakayepoteza ajira
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia: Msiogope mabadiliko, hakuna atakayepoteza ajira

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amewatoa hofu waajiriwa katika taasisi na mashirika ya umma yatakayofutwa kutokana na sababu mbalimbali kwamba watahamishiwa kwenye mashirika mengine kwani Serikali haiwezi kupoteza nguvu kazi yao. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya Ofisi ya msajili wa hazina kufanya uchambuzi na kubaini taasisi ambazo majukumu yanashabihiana na nyingine ambazo kwa sasa majukumu yake yamepitwa na wakati huku nyingine utendaji wake unalegalega.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Agosti 2023 wakati akifungua kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wa mashirika ya umma kinachofanyika jijini Arusha.

“Katika maboresho tunayoyafanya hakuna nguvukazi au ajira itakayopotea, wote ambao wapo kwenye mshirika aidha watamezwa kwingine au kutakuja mashirika mengine yenye maana sasa kuliko wakati yalipoanzishwa. Naomba msihofu msiogope mabadiliko yaliyopo,” amesema.

Amesema Serikali inafanya hivyo kwa sababu, takwimu zinaonesha asilimia 17 ya ajira nchini inatolewa na taasisi, mashirika na wakala hivyo haiwezi kuyaondoa ili ajira zipotee.

Amesema mpango huo utaipunguzia serikali gharama za uendeshaji na kuongezea ufanisi.

“Tumeambiwa mashirika haya ndio nguzo kuu ya maendeleo ya serikali, nguzo ya uchumi wa serikali. Yakizalisha wa vizuri Serikali inapata tija na kufanya makubwa zaidi, yakiwa mzigo inarudisha nyuma maendeleo ya serikali,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!