Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aonya taasisi, mashirika ya umma yanayokopa kutoa gawio
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia aonya taasisi, mashirika ya umma yanayokopa kutoa gawio

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema anataka kuona taasisi na mashirika ya umma yakichangia mfuko mkuu wa serikali kutokana na kipato kinachozalishwa kwa kutekeleza majukumu yao na sio kwenda kukopa ili kutoa gawio kwa Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Amesema anatambua kuwa kuna mashirika hayachangii chochote hadi sasa kwenye mfuko huo wa serikali kutokana na hali halisi ya mashirika hayo.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Agosti 2023 wakati akifungua kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wa mashirika ya umma kinachofanyika jijini Arusha.

“Wakati tulipolazimishwa kila shirika lazima litoe gawio natambua kwamba wakati ule unakuwa wakati mgumu kweli kwa Ma-CEO na bodi zao hadi wanaamua kwenda kukopa ilimradi tu wapeleke gawio kunusuru nafasi zao…  sasa kwa kuijua hali ile nikasema hapana.

“Wanaofanya faida walete gawio, wasiofanya faida tuwaangalie kwanini hawafanyi faida, kuna changamoto zipi na vikwazo vipi na tuwasaidie watoke huko waende wakazalishe walete faida hicho ndio tunachokwenda kufanya sasa,” amesema.

Aidha, amesema kutokana na mageuzi yanayokwenda kufanywa kwenye mashirika hayo, watendaji na wenyeviti wa bodi wajitafakari na kila mmoja aende akasimame kwenye nafasi yake sawasawa kwani mageuzi hayo ni ya lazima ili mashirika hayo yajiendeshe na serikali ipate faida.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!