Saturday , 30 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aonya taasisi, mashirika ya umma yanayokopa kutoa gawio
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia aonya taasisi, mashirika ya umma yanayokopa kutoa gawio

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema anataka kuona taasisi na mashirika ya umma yakichangia mfuko mkuu wa serikali kutokana na kipato kinachozalishwa kwa kutekeleza majukumu yao na sio kwenda kukopa ili kutoa gawio kwa Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Amesema anatambua kuwa kuna mashirika hayachangii chochote hadi sasa kwenye mfuko huo wa serikali kutokana na hali halisi ya mashirika hayo.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Agosti 2023 wakati akifungua kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wa mashirika ya umma kinachofanyika jijini Arusha.

“Wakati tulipolazimishwa kila shirika lazima litoe gawio natambua kwamba wakati ule unakuwa wakati mgumu kweli kwa Ma-CEO na bodi zao hadi wanaamua kwenda kukopa ilimradi tu wapeleke gawio kunusuru nafasi zao…  sasa kwa kuijua hali ile nikasema hapana.

“Wanaofanya faida walete gawio, wasiofanya faida tuwaangalie kwanini hawafanyi faida, kuna changamoto zipi na vikwazo vipi na tuwasaidie watoke huko waende wakazalishe walete faida hicho ndio tunachokwenda kufanya sasa,” amesema.

Aidha, amesema kutokana na mageuzi yanayokwenda kufanywa kwenye mashirika hayo, watendaji na wenyeviti wa bodi wajitafakari na kila mmoja aende akasimame kwenye nafasi yake sawasawa kwani mageuzi hayo ni ya lazima ili mashirika hayo yajiendeshe na serikali ipate faida.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!