Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia atangaza kufanya mabadiliko mawaziri, makatibu wakuu…
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atangaza kufanya mabadiliko mawaziri, makatibu wakuu…

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan ameutangazia umma wa Watanzania kuwa hivi karibuni atafanya mabadiliko ya nafasi za viongozi mbalimbali wa Serikali anayoiongoza kuanzia mawaziri, makatibu wakuu, wakurugenzi na wakuu wa mikoa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Januari, 2022 wakati akipokea maelezo kuhusu utekelezaji wa awali wa mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya Uviko 19.

Mpango huo ambao uliozinduliwa Oktoba mwaka jana, unatekelezwa kwa fedha za mkopo wa Sh. trilioni 1.3 kutoka Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwa kunufaisha sekta ya elimu, afya, maji, maliasili na utalii.

Aidha, akizungumzia kelele za wanaodai Serikali yake inakopakopa, amesisitiza hizo ni homa ya kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 hivyo atawaweka pembeni ili wakutane mbele ya safari.

“Nataka niwaambie nitatoa list mpya karibuni, wale wote ninaohisi wanaweza kwenda na mimi kwenye kazi ya maendeleo ya Watanzania, nitakwenda nao.

“Lakini wote ninaohisi ndoto zao ni kule na wanafanya kazi kwa ajili ya kule nitawapa nafasi waende wakajitayarishe vizuri huko nje, kwa sababu nikiwatuma ndani nitawasumbua kwa hiyo bora niwape nafasi wakajitayarishe tukutane huko mbele ya safari,” amesema.

Amesema lengo la Serikali ni maendeleo kwa watanzania hivyo viongozi anaowateua wanatakiwa kwenda kuleta maendeleo.

“Uongozi huletwa na Mungu aliyepangiwa ndiye atakayekaa,” amesema.

Amewaonya wakuu wa mikoa kuwa amewateua ili wamsaidie.

“Wakuu wa mikoa nimekuwekeni nikiamini kule nilikowakasimia madaraka mtakwenda kusimamia kazi na wengine wote kama vile makatibu wakuu na mawaziri.

“Nimekaa nadhani huu ni mwezi wangu wa nane sijui! nilisema nilikuwa nawasoma nanyi mnanisoma na siku nimefanya mageuzi kidogo ya mawaziri nikasema hapa nimeweka koma kazi inaendelea,” amesema.

1 Comment

  • Asante mama kwanza tunakupongeza kwa kutimiza wajibu wako uongozi kwa vitendo na matendo mabadiliko ya kimaendereo tunayaona wala hatuitaji kuwa tazameni asante mama jambo lamuhimu sasa ni kuwaondoa viongozi wasio tosheka na vyeo na wale wenye tamaa ya madaraka wengi wamejitokrza wazi wazi bira aibu .Mama ondoa shaka ktk shaka anaekuchikia mungu ampige lane anaekusaliti mungu ampige lana unapofanya kazi za taifa rais ufanye kwa usalama

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!