Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Rais Samia apongezwa uboreshaji huduma za afya Musoma Vijijini
Afya

Rais Samia apongezwa uboreshaji huduma za afya Musoma Vijijini

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amepongezwa kwa mchango mkubwa wa Serikali yake katika uboreshaji huduma za afya kwenye Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani Mara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Pongezi hizo zimetolewa hivi karibuni na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru, Abdalla Shaibu Kaim, akikagua utekelezaji wa miradi ya sekta ya afya, jimboni humo, ambaye aliambatana na timu yake.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, imesema amewapongeza viongozi wa jimbo hilo pamoja na wananchi kwa kazi kubwa wanayofanya kuanza utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa nguvu zao, kisha kuungwa mkono na Serikali.

“Kaim na timu yake yote wameipongeza sana Serikali na Rais Samia , kwa kutoa michango mikubwa ya kifedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo Musoma Vijijini. Vilevile, Wananchi na viongozi wao wa Chama na Serikali Musoma Vijijini wamepongezwa kwa kazi nzuri wazifanyazo kwenye utekelezaji ya miradi ya maendeleo ya vijijini mwao,” imesema taarifa hiyo.

Miongoni mwa miradi ambayo wananchi wa jimbo hilo wanashirikiana na Serikali kuitekeleza ni hospitali moja ya hadhi ya wilaya, katika Kitongoji cha Kwikonero, vituo sita vya afya, zahanati 41.

Pia, mbunge wa jimbo hilo, Prof. Muhongo amegawa magari matano ya kusafirishia wagonjwa (Ambulances).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

error: Content is protected !!