RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemuondoa aliyekuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Mabasi Yaendayo Haraka (UDART), Gilliard Wilson Ngewe na kumteua Waziri Kindamba, kuiongoza kampuni hiyo ya usafirishaji. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Taarifa ya uteuzi huo imetolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Moses Kusiluka leo tarehe 9 Machi 2024.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Zuhura, Ngewe atapangiwa kazi nyingine.
“Waziri Kindamba aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa UDART. Kindamba anachukua nafasi ya Ngewe ambaye atapangiwa kazi nyingine,” imesema taarifa hiyo.
Ngewe aliiongoza kampuni hiyo kuanzia Oktoba 2023, alipoteuliwa.
Leave a comment