Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia amliza mjane wa Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia amliza mjane wa Magufuli

Spread the love

MANENO ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, juu ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dk. John Magufuli imemliza  mjane wake, Janeth Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Tukio hilo limetokea jana tarehe 5 Novemba 2023, wakati Rais Samia akizindua nyumba mpya ya Hayati Magufuli ambaye alikuwa mtangulizi wake, iliyojengwa na Serikali, jijini Dar es Salaam.

Mama Janeth alijikuta anaatokwa machozi wakati alipomkumbatia Rais Samia, pia baadhi ya wanafamilia yake walijikuta wakilia wakati kiongozi huyo anatoa hotuba yake.

Wakati akitoa hotuba yake, Rais Samia alimuomba Mama Janeth akubali kupokea nyumba hiyo kwa niaba ya Hayati Magufuli, ambaye amemtaja kama mlezi na kaka yake.

“Ndugu yangu Janeth, nikiwa na mchanganyiko wa hisia naomba leo (jana) uridhie kupokea nyumba hii kwa niaba ya mpendwa wetu, kaka yangu, boss wangu na mlezi wangu, Hayati Magufuli,” alisema Rais Samia.

Katika hatua nyingine, Rais Samia aliagiza wake wa viongozi ambao wametangulia mbele ya haki, watunzwe kwa kuwa walilitumikia taifa wakati wenza wao wako madarakani.

“Hawa watu ni haki yao watunzwe, walilitumikia taifa wakati waume zao wako kazini na wenyewe walitumikia taifa. Waume wamewaacha ni lazima tuwatunze,” alisema Rais Samia.

Kwa upande wake Mama Janeth, alimshukuru Rais Samia akisema “mheshimiwa Rais tendo ulilofanya litabaki kuwa lililotukuka na alama isiyofutika kioyoni mwetu ukizingatia kuwa nyumba hii itakuwa ndiyo makazi ya kudumu ya familia. Nakushukuru sana mama ubarikiwe.”

“Kitendo hiki ulichotutendea katika familia ya Hayati Magufuli ni dhahiri kwamba umeniachia deni, nikiwa kama mama wa familia hii zawadi pekee ninayoweza kukuahidi ni kukuombea mema daima kwa mola wetu ili Mungu aendelee kukupigania na kukubariki na kukujalia maisha mema na kazi unayofanya,” alisema Mama Janeth

Hayati Magufuli alifariki dunia akiwa madarakani kwa ugonjwa wa umeme, tarehe 17 Machi 2021 na mwili wake ulizikwa kijijini kwao Chato mkoani Geita. Wakati anafariki, Rais Samia alikuwa makamu wake wa Rais.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!