Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aanika idadi ya majengo, yapo ya shule na afya
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia aanika idadi ya majengo, yapo ya shule na afya

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

NCHI ya Tanzania, ina majengo 14,348,372 (milioni 14.3), ambapo Bara kuna majengo 13,907,951 na Zanzibar 440,421. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Takwimu hizo zimetolewa leo Jumatatu, tarehe 31 Oktoba 2022, jijini Dodoma na Rais Samia Suluhu Hassan, akitangaza matokeo ya sensa ya watu na makazi ya 2022, iliyofanyika Agosti mwaka huu.

Rais Samia amesema, majengo ya kutolea huduma za afya yako 10,067, kati ya hayo 7,889 ni ya zahanati, wakati ya vituo vya afya yakiwa 1,490 huku ya hospitali yakiwa ni 688.

“Upande wa elimu, matokeo yanaonyesha Tanzania ina jumla ya shule 25,626, ambapo shule za msingi ni 19,769 na shule za sekondari ni 5,857. Ndugu wananchi idadi yetu kwa sasa ni kama nilivyotaja,” amesema Rais Samia.

Kwa mujibu wa matokeo ya sensa ya watu na makazi iliyotangazwa na Rais Samia, majengo hayo yanahudumia watu 61,741,120.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!