Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Mwinyi afuta sherehe za mapinduzi 2022
Habari Mchanganyiko

Rais Mwinyi afuta sherehe za mapinduzi 2022

Spread the love

RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein Mwinyi, amesema  2022 hakutakuwa na sherehe za kitaifa za maadhimisho ya miaka 59 ya mapinduzi ya visiwa hivyo, badala yake fedha zilizopangwa kutekelezea shughuli hizo, zitapelekwa kwenye sekta ya elimu.Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Rais Mwinyi ametoa uamuzi huo leo Jumamosi, tarehe 31 Desemba 2022, akitangaza ratiba ya wiki ya maadhimisho ya miaka 59 ya mapinduzi ya Zanzibar, itakayoanza tarehe 1 hadi 12 Januari 2023.

“Mwaka huu kama Serikali tumeamua Serikali kupeleka fedha zilizopangwa kwenye kilele cha sherehe za mapinduzi mwaka huu katika sekta ya elimu ili skuli zetu ziwe na vifaa vya kutosha kuanzia madawati, maabara na maktaba ili tunapokuwa tunazindua skuli nyingi na madarasa mengi, si vyema ziwe hazina dhana zinazotakiwa,” amesema Rais Mwinyi.

Mbali na sababu hiyo, Rais Mwinyi amesema sababu nyingine ya kuahirisha sherehe hizo, ni kujipanga kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 60 ya mapinduzi ya Zanzibar.

“Siku ya kilele huwa tunakuwa na gwaride katika uwanja wa Amani, safari hii haitakuwepo sababu tumeona Serikali tujipange katika maadhimisho kwa jambo kubwa zaidi mwaka ujao ambapo mapinduzi yetu yatafikia miaka 60. Sherehe zitakuwa kubwa zaidi na mambo mengi kuliko kawaida. Kwa maana hiyo Serikali itajipanga kibajeti ili kuweza kutimiza maadhimisho ya mwaka ujao,” amesema Rais Mwinyi.

Katika hatua nyingine, Rais Mwinyi amesema kwenye wiki ya maadhimisho ya sherehe za mapinduzi, miradi takribani 55 itazinduliwa. Hata hivyo, hakutaja kiasi cha fedha ambacho kitapelekwa katika sekta ya elimu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!