Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi wazuia mkutano wa Maalim Seif Temeke
Habari za Siasa

Polisi wazuia mkutano wa Maalim Seif Temeke

Maalim Seif Shariff Hamad akikabishiwa kadi alipojiunga na ACT-Wazalendo
Spread the love

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimezuiwa kufanya mkutano wake wa ndani na Jeshi la Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke kutokana na kukosa kibali. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Chama hicho kilipanga kufanya mkutano wa ndani wa kuwajengea uwezo viongozi wake wa kata, katika ukumbi wa Hoteli ya Sunrise iliyoko Temeke jijini Dar es Salaam ambapo Maalim Seif Shariff Hamad, Mshauri wa ACT-Wazalendo, alitarajiwa kufungua mkutano huo.

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 24 Agosti 2019 na Ray Matata, Katibu wa Itikadi na Uenezi ACT-Wazalendo mkoa wa Dar es Salaam wakati akizungumza na MwanaHALISI Online kwa njia ya simu.

Matata amesema asubuhi ya leo askari polisi walifika katika ofisi za chama hicho, Kata ya Azimio na kuwaeleza viongozi waliokuwepo hapo kwamba hawaruhisiwi kufanya mkutano huo kwa sababu hawana kibali cha polisi.

“Tulikuwa na tukio la uzinduzi wa matawi na mkutano wa ndani wa kichama wa kuwajengea uwezo viongozi wa matawi, mshauri wa chama angekuja kufungua, wamekuja polisi na kuzuia wakisema kwamba mkutano wa ndani unatakiwa kuwa na kibali, wamesema hatuna kibali zimekuja gari za kutosha zimezuia ofisi ya Kata ya Azimio,” amesema Matata.

Aidha, Matata amesema wanaendelea kufuatilia suala hilo, na kisha watatoa taarifa kamili kwa umma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!