Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi wauwa watu wanne
Habari Mchanganyiko

Polisi wauwa watu wanne

SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Kanda Maalum Dar es Salaam
Spread the love

JESHI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limeuwa watu wanne kwa risasi wakidai kuwa ni majibizano. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo terehe 18 Agosti 2020 na Kamanda wa Jeshi la Polisi kanda hiyo, SACP Lazaro Mambosasa kupitia taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari.

Mambosasa amesema, jeshi hilo limeuwa watu hao kwenye majibizano ya risasi saa 9:30 tarehe 15 Agosti 2020 .

“…tulifanikiwa kukamata silaha moja bastola aina ya Bereta iliyofutwa namba zake za usajili ikiwa na risasi moja ndani ya magazine na maganda manne ya risasi, tochi moja na milipuko miwili iliyotengenezwa kienyeji,” amesema Mambosasa.

Amesema, awali jeshi hilo lilimshikilia Nuru Thadei (34), aliyetajwa kuhusika na matukio ya uhalifu ikiwa pamoja na tukio la mauaji ya mchina mwaka 2011 eneo la Kurasini, jijini Dar es Salaam.

Mambosasa amesema, Thadei alivyohojiwa, alikiri kuhusika na matukio hayo na kuwaongoza askari wa jeshi hilo mpaka kwenye nyumba ya maficho ya wenzike watatu.

Baada askari kufika eneo hilo, Thadei alipiga kelele ya kutoa ishara kwa wenzake na ndio walipoanza kurusha risasi kuelekea walipo askari, walijibu na kusababisha kujeruhi watu hao ambapo kabla ya kufikishwa hospitali, walishafariki dunia.

Mbali na Thadei, wengine ni pamoja na Godfrey Faustine, Antony Mnyamongo na Peter Mseba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!