Tuesday , 3 October 2023
Habari za SiasaTangulizi

Polisi wamsaka Kigogo

Spread the love

 

JESHI la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Dar es Salaam linamsaka mwanaharakati anayejiita jina la Kigogo katika mtandao wa Twitter. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

‘Mwanaharakati’ huyo anadaiwa kuzusha hofu baada ya kusambaza taarifa za uongo, kwamba Rais John Magufuli anaumwa.

Taarifa hiyo imetolewa na Ramadhani Kingai, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kinondoni leo Jumamosi tarehe 13 Machi 2021, wakati akizungumza na vyombo vya habari mkoani Dar es Salaam.

Kamanda Kingai amesema, jeshi hilo linaendelea kumfuatilia Kigogo, na kwamba wakati wowote litamkamata kujibu tuhuma zinazomkabili za kumzushia ugonjwa Rais Magufuli.

“Bado tunaendelea kufuatilia taarifa za wengine ambao wanasambaza taarifa za kizushi, yeyote atakayesambaza tunapekua kila sehemu, tutazifanyia kazi kuhakikisha wanaohusika wanachukuliwa hatua za kisheria.

“Huyu anayeitwa  Kigogo ni mhalifu kama wengine, tunaendelea kupekua kuhakikisha na yeye tunamtia mbaroni. Muda, siku haijafahamika ila tutamkamata tu,” ameahidi Kamanda Kingai.

 

Taarifa zinazodai Rais Magufuli mgonjwa, zilianza kusambazwa mitandaoni hasa twitter mapema wiki hii.

Hata hivyo, jana tarehe 12 Machi 2021 akiwa mkoani Njombe, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alikanusha madai hayo.

Alisema, Rais Magufuli yupo buheri wa afya na haonekani hadharani kwa sababu, anatekeleza majukumu yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mobhare Matinyi Msemaji mpya wa Serikali

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa Mkuu wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Basi la Magereza lagonga treni yenye abiria 650 Dar

Spread the loveBasi  Jeshi la Magereza lenye namba MT 0040 limegonga treni...

error: Content is protected !!