Saturday , 27 April 2024
Habari za SiasaTangulizi

Polisi wamsaka Kigogo

Spread the love

 

JESHI la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Dar es Salaam linamsaka mwanaharakati anayejiita jina la Kigogo katika mtandao wa Twitter. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

‘Mwanaharakati’ huyo anadaiwa kuzusha hofu baada ya kusambaza taarifa za uongo, kwamba Rais John Magufuli anaumwa.

Taarifa hiyo imetolewa na Ramadhani Kingai, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kinondoni leo Jumamosi tarehe 13 Machi 2021, wakati akizungumza na vyombo vya habari mkoani Dar es Salaam.

Kamanda Kingai amesema, jeshi hilo linaendelea kumfuatilia Kigogo, na kwamba wakati wowote litamkamata kujibu tuhuma zinazomkabili za kumzushia ugonjwa Rais Magufuli.

“Bado tunaendelea kufuatilia taarifa za wengine ambao wanasambaza taarifa za kizushi, yeyote atakayesambaza tunapekua kila sehemu, tutazifanyia kazi kuhakikisha wanaohusika wanachukuliwa hatua za kisheria.

“Huyu anayeitwa  Kigogo ni mhalifu kama wengine, tunaendelea kupekua kuhakikisha na yeye tunamtia mbaroni. Muda, siku haijafahamika ila tutamkamata tu,” ameahidi Kamanda Kingai.

 

Taarifa zinazodai Rais Magufuli mgonjwa, zilianza kusambazwa mitandaoni hasa twitter mapema wiki hii.

Hata hivyo, jana tarehe 12 Machi 2021 akiwa mkoani Njombe, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alikanusha madai hayo.

Alisema, Rais Magufuli yupo buheri wa afya na haonekani hadharani kwa sababu, anatekeleza majukumu yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!