ESHI la Polisi Wilaya ya Kilwa Mkoa wa Lindi, limemkamata Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama siasa cha ACT-Wazalendo. Anaripoti Faki Sosi, Kilwa…(endelea)
Zitto amekamatwa leo Jumanne asubuhi tarehe 23 Juni 2020 akiwa anajiandaa kuongoza kikao cha ndani cha wanachama wa chama hicho.
Kikao hicho, kilikuwa kinafanyikia ukumbi wa Stamford Bridge ulipo Kilwa Masoko.
Mbali na Zitto, wengine waliokamatwa ni Mbunge wa Kilwa Kusini, Seleman Mbungara maarufu ‘Bwege’ na Sheweji Mketo ambaye niKatibu wa Kamati ya Oganaizesheni ya chama hicho.
Zitto yuko katika ziara katika mikoa ya Kusini aliyoianza jana Jumatatu.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE na MwanaHALISI TV kwa habari zaidi
Leave a comment