Thursday , 7 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Milioni 9 waambukizwa corona duniani
Kimataifa

Milioni 9 waambukizwa corona duniani

Spread the love

MAAMBUKIZO ya ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona (COVID-19) duniani, yamefikia milioni 9.19 huku waliopona wakiwa milioni 4.94. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa ‘worldometer’ leo Jumanne tarehe 23 Juni 2020 unaonyesha vifo vinavyotokana na ugonjwa huo vimefikia 474,479.

Marekani ni Taifa linaloongoza kwa maambukizo mengi ya watu milioni 2.38, waliopona wakiwa milioni moja huku vifo vikiwa  122,611.

Brazil ina wagonjwa milioni 1.1, vifo 51,407 huku waliopona ugonjwa huo wakiwa 594,104.

China ambako ugonjwa huo ulianzia mwishoni mwa mwaka 2019, kuna wagonjwa 83,418, waliofariki dunia wakiwa 4,634 na waliopona ni 78,425.

Nchini Kenya, maambukizo yamefikia 4,797, waliopona 1,680, waliofariki dunia wakiwa 125 huku idadi ya sampuli zilizokwisha kupimwa ni 142,366

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!