JESHI la Polisi wilayani Kigoma limemzuia Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini, kufanya mkutano wake wa hadhara na wananchi, leo tarehe 17 Januari 2020, kwenye Viwanja vya Mwanga Center, Manispaa ya Kigoma Ujiji. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).
Kwa mujibu wa barua iliyotolewa na SSP Mayunga Mayunga, Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilayani Kigoma, mkutano huo umezuiwa kwa sababu za kiusalama, kutokana na taarifa za kiintelijensia ilizopata jeshi hilo.
“Napenda kukujulisha kuwa mkutano huo umezuiliwa kwa tarehe uliyoomba, kwa sababu za kiusalama kutokana na taarifa za kiintelejensia zilizopo. Kwa hiyo hauruhusiwi kufanya mkutano au kuendelea na maandalizi ya mkutano huo,” inaeleza sehemu ya barua hiyo.
Kufutia hatua hiyo, Zitto amesema sababu zilizotolewa na jeshi hilo kuhusu mkutano huo kuzuiwa, hazikuwa za msingi.
“Polisi wamezuia mkutano wetu wa Hadhara wa Mbunge. Jana jioni Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini amepata barua hii ya Polisi kuzuia Mkutano halali wa Mbunge kuzungumza na Wananchi wake. Sababu zilizotolewa ni za kipuuzi ‘intelijensia’,” ameandika Zitto katika ukurasa wake wa Twitter.
Polisi wamezuia mkutano wetu wa Hadhara wa Mbunge. Jana jioni Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini amepata barua hii ya Polisi kuzuia Mkutano halali wa Mbunge kuzungumza na Wananchi wake. Sababu zilizotolewa ni za kipuuzi ‘intelijensia’. @MwananchiNews @Uhurubilamipaka pic.twitter.com/JiLcxjJ5u9
— Zitto MwamiRuyagwa Kabwe (@zittokabwe) January 17, 2020
Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, amesema mkutano huo ulilenga kuzungumzia maendeleo ya wananchi wa jimbo lake, pamoja na changamoto ya huduma ya usajili wa vitambulisho vya taifa, inayotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho nchini (NIDA).
Leave a comment