Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Polisi, Dawasco, Tanesco kuanzisha msako mkali
Habari Mchanganyiko

Polisi, Dawasco, Tanesco kuanzisha msako mkali

Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Tanesco, Dawasco na kampuni mbalimbali za simu za mkononi limeanzisha msako dhidi ya watu wanaohujumu miundombinu ya mashirika hayo. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema kuanzia tarehe 27 Agosti mwaka huu, litafanya operesheni hiyo kali itaanza kuhakikisha mtandao wa wizi huo unaisha.

“Kumekuwa na wimbi kubwa la watu kujiunganishia maji safi kutoka kwenye mabomba ya DAWASCO bila kufuata utaratibu, pia wanaojiunganishia umeme kinyume na utaratibu, kuiba mafuta ya transformer na kuiba betri kwenye minara ya kampuni za simu hapa jijini Dar es Salaam,” amesema.

Aidha Mambosasa amesema Jeshi la Polisi kuanzia sasa linawataka watu wote wanaojihusisha na uhalifu huo kuacha mara moja  na kujisalimisha wenyewe  katika vituo vya Polisi au katika mashirika na kampuni hizo kabla ya kuanza kwa oparesheni hiyo kali, na watakaokaidi agizo hili watakamatwa na kufunguliwa mashtaka ya uhujumu uchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!