Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi, Dawasco, Tanesco kuanzisha msako mkali
Habari Mchanganyiko

Polisi, Dawasco, Tanesco kuanzisha msako mkali

Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Tanesco, Dawasco na kampuni mbalimbali za simu za mkononi limeanzisha msako dhidi ya watu wanaohujumu miundombinu ya mashirika hayo. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema kuanzia tarehe 27 Agosti mwaka huu, litafanya operesheni hiyo kali itaanza kuhakikisha mtandao wa wizi huo unaisha.

“Kumekuwa na wimbi kubwa la watu kujiunganishia maji safi kutoka kwenye mabomba ya DAWASCO bila kufuata utaratibu, pia wanaojiunganishia umeme kinyume na utaratibu, kuiba mafuta ya transformer na kuiba betri kwenye minara ya kampuni za simu hapa jijini Dar es Salaam,” amesema.

Aidha Mambosasa amesema Jeshi la Polisi kuanzia sasa linawataka watu wote wanaojihusisha na uhalifu huo kuacha mara moja  na kujisalimisha wenyewe  katika vituo vya Polisi au katika mashirika na kampuni hizo kabla ya kuanza kwa oparesheni hiyo kali, na watakaokaidi agizo hili watakamatwa na kufunguliwa mashtaka ya uhujumu uchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!