Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Njama za kuvuruga mkutano KKKT zafichuka
Habari za SiasaTangulizi

Njama za kuvuruga mkutano KKKT zafichuka

Mkuu wa KKKT, Dk. Fredrick Shoo
Spread the love

KUNA njama zinasukwa za kutaka kuvuruga mkutano mkuu wa Kanisa Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), kupitia kinachoitwa, “Kanisa Moja, Katiba Moja.” Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Taarifa kutoka Arusha zinasema, baadhi ya viongozi wanalazimisha kuwapo mabadiliko ya Katiba yanayolenga kuifanya KKKT kuwa na katiba moja, hoja ambayo inapingwa na wajumbe waliowengi.

Mpango wa Kanisa Moja, Katiba Moja, unadaiwa unalenga kumbeba Dk. Shoo, ili aweze kuendelea kuwa kiongozi wa kanisa hilo.

“Kuna watu wanataka kuvuruga mkutano wetu kwa kulazimisha Kanisa hili kuwa na Katiba moja. Nakuambia hivi, hatukubali. Hii ajenda ililetwa Shinyanga mwezi uliyopita, tukaikataa. Hatuwezi kuipitisha sasa,” ameeleza mjumbe mmoja wa mkutano mkuu wa KKKT unaofanyika jijini Arusha.

Anaongeza, “tunajua nani yuko nyuma ya mpango huu. Tunajua ni kipi kinacholengwa. Tunajua. Ni bora mkutano kuvurugika, kuliko kupitisha jambo hili.”

Mwandishi ameshindwa kumpata Askofu Shoo, kuzungumzia kadhia hiyo. Anaendelea kumtafuta.

Mara kadhaa katika maadhimisho ya miaka 60 ya KKKT, Askofu Dk. Shoo aliwalaumu wanaopinga mpango huo mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!