Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NCCR-Mageuzi yakubali kushiriki mkutano TCD na Rais
Habari za SiasaTangulizi

NCCR-Mageuzi yakubali kushiriki mkutano TCD na Rais

Edward Sembeye, Mkuu wa Idara ya Uenezi na Mahusiano ya Umma wa NCCR Mageuzi
Spread the love

 

CHAMA cha NCCR-Mageuzi, kimetengua azimio lake la kutoshiriki mkutano wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na Rais Samia Suluhu Hassan, baada ya mapendekezo yake kufanyiwa kazi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Ijumaa, tarehe 11 Machi 2022, jijini Dar es Salaam, na Mkuu wa Idara ya Uenezi na Mahusiano ya Umma Taifa, Edward Simbeye, akitangaza maazimio ya Kamati Kuu ya chama hicho, iliyoketi jana jijini humo.

“Kamati kuu imezingatia mambo hayo na imejiridhisha hoja zote kinzani tulizotoa zimezingatiwa na kwa msingi huo hatutakuwa na sababu yoyote ya kutoshiriki mkutano wa majadiliano ya amani kule Dodoma tarehe 30 na 31, Machi 2022,” amesema Simbeye.

Simbeye amesema, “Kamati Kuu imekubali kutengua azimio lake la kutoshiriki na sisi NCCR-Mageuzi tutashiriki kama wanachama halali wa TCD, lakini mambo tuliyokubaliana yametekelezwa pasi na shaka. Hivyo tutashiriki.”

Mkuu huyo wa Uenezi NCCR-Mageuzi, ametaja miongoni mwa mapendekezo yao yaliyofanyiwa kazi, ikiwemo ya Rais Samia kukubali kufanya mkutano wa awali na wadau wa vyama vya siasa kabla ya mkutano huo.

Simbeye amesema, Rais Samia atafanya mkutano na viongozi wa vyama vya siasa tarehe 18 Machi mwaka huu, ambapo NCCR-Mageuzi itawakilishwa na Mwenyekiti wake, James Mbatia.

“Tulisema ili tushiriki tukiwa na amani kuwe na mkutano mdogo wa vyama vya siasa vinavyounda TCD pamoja na Rais, tunaamini katika kweli, tuzungumze, tutibiane makovu ya uchaguzi, tuzungumze uso kwa uso kabla ya kwenda kwa umma,” amesema Simbeye.

NCCR-Mageuzi, kilikataa kushiriki mkutano wa wadau wa vyama vya siasa ulioandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, na kufanyika Desemba 2021 jijini Dodoma, ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais Samia.

Chama hicho kiligoma kushiriki mkutano huo kikitaka maridhiano juu ya changamoto zilizojitokeza kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2020.

Simbeye amesema, NCCR-Mageuzi kinahitaji muafaka wa kitaifa na Tanzania iliyo salama na yenye amani

“Tunataka kila mtu apate haki yake, ndiyo maana tulikuwa tunasimamia haki. Pale ambapo kuna haki tunasimamia haki, pale ambapo hakuna haki hatutakuwa wavivu kusema hapa hakuna haki na tutatoa njia ya kupata haki,” amesema Simbeye na kuongeza:

“Ndiyo maana tumekubaliana kwamba kuna mwanga wa kushirki mkutano huu na baada ya hapo majadiliano mengine yataendelea.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!