Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo NBC Benki yawapa fursa wakazi wa Mwanza kulishuhudia kombe la Ligi kuu ya NBC
Michezo

NBC Benki yawapa fursa wakazi wa Mwanza kulishuhudia kombe la Ligi kuu ya NBC

Spread the love

Wadhamini wakuu wa ligi ya Tanzania bara maarufu kama Ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya Biashara(NBC), imewapelekea wakazi wa jiji la Mwanza kombe jipya la ubingwa wa ligi hiyo namba tano kwa ubora barani Afrika. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Baadhi ya mashabiki na wapenda soka wa mkoa wa Mwanza wakipiga picha na kombe la ligi kuu ya NBC ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa benki ya NBC ambayo ni mdhamini mkuu wa ligi ya soka Tanzania bara kuwapelekea  wateja wake pamoja na mashabiki wa soka kombe hilo na kuwapa fursa ya kuliona na kupiga nalo picha.

Kwa mujibu wa NBC, lengo la kulipeleka kombe hilo mkoani Mwanza, ni kuwapa fursa wateja wa benki hiyo, wapenzi wa soka na wakazi wa jiji hilo kwa ujumla, fursa ya kulishuhudia na kupiga nalo picha kombe hilo jipya.

Baadhi ya mashabiki na wapenda soka wa mkoa wa Mwanza wakilishuhudia kombe la ligi kuu ya NBC ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa benki ya NBC ambayo ni mdhamini mkuu wa ligi ya soka Tanzania bara kuwapelekea  wateja wake pamoja na mashabiki wa soka kombe hilo na kuwapa fursa ya kuliona na kupiga nalo picha.

Shughuli ya kulishuhudia kombe, imeenda sambamba na fursa ya kupata huduma mbalimbali za kibenki kwa wakazi wa jiji hilo kutoka katika benki hiyo kongwe na yenye mtandao mpana wa matawi hapa nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!