Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwanza yatekeleza miradi ya maji ya 788 Bil
Habari Mchanganyiko

Mwanza yatekeleza miradi ya maji ya 788 Bil

Bomba la maji
Spread the love

JUMLA ya miradi 17 ya kimkakati katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, yenye thamani ya Sh. 788 bilioni inaendelea kutekelezwa. Anaripoti Moses Mseti, Mwanza … (endelea).

Lengo la kutekelezwa kwa miradi hiyo ni kutatua kero ya muda mrefu ya maji, inayowakabili baadhi ya wananchi wa mikoa hiyo wanaotumia maji ya visima.

Kauli hiyo imetolewa na Prof. Kitila Mkumbo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji alipotembelea chanzo cha maji cha Nyahiti, likichopo Mapilinga wilayani Misungwi na baadaye kufanya mkutano wa hadhara kwenye eneo la Kisesa, Magu.

Miradi hiyo inatekelezwa na serikali kupitia Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira jijini Mwanza (Mwauwasa).

“Serikali inataka kumaliza kero ya maji na kuwa historia, inatekeleza miradi 17 ya kimkakati Kanda ya  Ziwa kwa gharama ya shilingi bilioni 788 na itatumia maji ya ziwa hilo.

“Serikali imelivalia njuga tatizo la maji na sisi tutahakikisha linatatuliwa, hivyo mnapotuhukumu, angalieni tumetoka wapi na nini tunakifanya,” amesema Prof. Mkumbo.

Prof. Mkumbo amesema, wizara yake inatekeleza miradi mitatu katika Wilaya za Misungwi, Magu na Mji wa Lamadi wilayani Busega.

Pia amesema, kutokana na changamoto hiyo serikali imeanza kuchukua hatua za haraka kuhakikisha wananchi wa Kisesa, Bujora na Bukandwe wanapata maji ifikapo tarehe 15 Novemba mwaka huu, na miezi sita baadaye ujenzi wa tanki kubwa la maji utakuwa umekamilika.

“Kero ya maji ni kubwa na serikali hatua inazochukua kutatua kero hiyo si ahadi, inataka kupanua mtandao wa maji hapa Kisesa na kwingine ili kumaliza tatizo hilo kwa miaka mingi.,”alisema Profesa Mkumbo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!