Saturday , 10 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Papa aridhia Kadinali Pengo kustaafu, Askofu Ruwa’ichi ampokea
Habari Mchanganyiko

Papa aridhia Kadinali Pengo kustaafu, Askofu Ruwa’ichi ampokea

Spread the love

OMBI la Kadinali Polycarp Pengo, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam kung’atuka madarakani, limeridhiwa na Papa Francisko. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Papa Francisko amebariki ombi la Kadinali Pengo kuondoka madarakani alipokuwa kwenye maadhimisho ya Sherehe ya Bikira Maria Kupalizwa Mbinguni.

Hata hivyo, Papa Francisko amemteua Askofu mkuu mwandamizi, Yuda Thaddeus Ruwa’ichi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam kuchukua nafasi ya Kadinali Pengo kuanzia sasa.

“Katika maadhimisho ya Sherehe ya Bikira Maria Kupalizwa Mbinguni, mwili na roho, tarehe 15 Agosti 2019, Baba Mtakatifu Francisko ameridhia ombi la Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, Tanzania la kung’atuka kutoka madarakani,” imeeleza taarifa ya Padre Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC).

Hivi karibuni, Kadinali Pengo katika maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 75 tangu kuzaliwa kwake, aliwaambia watu wa Mungu Jimbo Kuu la Dar es Salaam kwamba, anasubiria wakati wowote kumtii Baba Mtakatifu Francisko atakapomwambia kupumzika katika utume wa Kiaskofu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!