Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Mwanafunzi kidato cha 3 ajinyonga darasani, akutwa na ujumbe wa kugomea shule
ElimuTangulizi

Mwanafunzi kidato cha 3 ajinyonga darasani, akutwa na ujumbe wa kugomea shule

Spread the love

MWANAFUNZI wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Lumbira kata ya Luanda wilayani Mbozi mkoani Songwe,Japhari Mwashitete  (16) amekutwa amefariki dunia kwa kujinyonga darasani.

Mwili wa mwanafunzi huyo umekutwa ukiwa na ujumbe wa  kuikataa shule hiyo. Anaripoti Ibrahim Yassin…(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jana tarehe 4  Julai 2023, Kamanda wa polisi mkoani Songwe, Theopista Mallya amesema wamepokea taatifa za kuiinyonga mwanatunzi huyo juzi tarehe 3 Julai 2023 muda wa saa 10 jioni.

RPC Mallya

Amefafanua kuwa polisi walifanya taratibu za vipimo vya daktari na kubaini amekufa kwa kujinyonga hivyo polisi wakaamua kuruhusu familia kuendelea na taratibu za mazishi. 

Kamanda Malya amesema baada ya kifo hicho waliangalia kwenye mfuko wa suruali ya mwanafunzi huyo na kukuta karatasi yenye maandishi yenye ujumbe wa kukataa kusoma shule ya Lumbira na badala yake anataka kusoma shule ya Myovizi iliyopo kilometa chache kutoka shule hiyo

Amesema kufuatia tukio hilo hakuna mtu ama watu waliokamatwa wakihusishwa na tukio hilo huku jeshi lake likiendelea na uchunguzi wa kina kuona kama kuna mtu ama watu wamehusika na tukio hilo. 

Kufuatia tukio hilo wananchi wanaozunguka eneo hilo wamesikitishwa na kitendo cha mwanafunzi huyo kuchukua maamuzi hayo magumu huku wakitaka uchunguzi zaidi ufanyike kuona kama kuna mtu kahusika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

error: Content is protected !!