Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwalimu wa madrasa ahukumiwa miaka 80 jela kwa ubakaji
Habari Mchanganyiko

Mwalimu wa madrasa ahukumiwa miaka 80 jela kwa ubakaji

Spread the love

 

MUSSA Nassibu Ismail (21), mwalimu wa madrasa iliyopo maeneo ya Kiboje wilayani Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, amehukumiwa kifungo cha miaka 80 gerezani au faini ya Sh. 3,000,000, baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mtoto wa kike wa miaka 15. Anaripoti Noela Shila, TUDARCO … (endelea).

Hukumu hiyo imetolewa jana tarehe 17 Agosti 2021 na Mahakama ya Mkoa wa Mwera visiwani Zanzibar, mbele ya Hakimu Said Hemed Khalfan.

Akitoa hukumu ya kesi hiyo iliyokuwa na mashtaka manne, Hakimu Khalfan amesema mshtakiwa huyo amehukumiwa kifungo cha miaka 30 kwa kila kosa, katika mashtaka mawili ya ubakaji yanayomkabili.

Huku, akihukumiwa kifungo cha miaka 10 kwa kila kosa, katika mashtaka mawili yanayomkabili ya kumtorosha mtoto huyo.

Hivyo, jumla ya muda wa kifungo ni miaka 80, lakini mshtakiwa huyo atatumikia kifungo cha miaka 30 pekee, kwa kuwa adhabu hiyo inakwenda kwa pamoja.

Hakimu Halfani alisema, mshtakiwa huyo alifanya makosa hayo kati ya Oktoba 18 na Novemba 2, 2019, katika madrasa iliyoko maeneo ya Kiboje visiwani humo.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!