Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali yakwama kuzuia kesi ya kupinga malipo elimu juu
Elimu

Serikali yakwama kuzuia kesi ya kupinga malipo elimu juu

Mahakama Kuu ya Tanzania
Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, imetupilia mbali mapingamizi ya Serikali, katika kesi Na. 16/2021, iliyofunguliwa na Alexandra Bakunguza, kupinga elimu ya juu kutolewa kwa malipo. Anaripoti Noela Shila, TUDARCo … (endelea).

Mapingamizi hayo yalitupwa na mahakama hiyo, jana Jumanne tarehe 17 Agosti 2021, mbele ya Jaji Modesta Opiyo.

Serikali iliwasilisha mapingamizi matatu katika kesi iliyofunguliwa na mhitimu huyo wa Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira (TUMa), jijini Arusha, tarehe 29 Julai 2021kwa madai kwamba haina mashiko.

Jaji Opiyo alikataa mapingamizi hayo, akidai kwamba yanaingia kwenye kiini cha msingi wa kesi, kinyume cha mapingamizi ya awali yanavyopaswa kufanyika.

Charles Kichere, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)

Kufuatia hatua hiyo, mahakama hiyo itaendelea na usikilizwaji wa kesi hiyo, ambapo imepanga kuisikiliza tarehe 2 Septemba 2021.

Bakunguza amefungua kesi hiyo, dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB).

Mhitimu huyo wa chuo kikuu, anaomba wanafunzi wasilipishwe gharama za masomo ya elimu ya juu, badala yake Serikali ibebe jukumu hilo.

Katika kesi hiyo, anapinga elimu ya juu kugharamiwa na Serikali kwa njia ya mkopo, kinyume na Ibara ya 11 ya katiba ya Tanzania, ambayo inayoelekeza Seriali itoe elimu na mafunzo ya ufundi kwenye ngazi zote kwa usawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!