Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mwakyembe atoa sababu 10 za kuhamia CCM
Habari za Siasa

Mwakyembe atoa sababu 10 za kuhamia CCM

Spread the love

ALIYEKUWA Diwani wa Mtoni kwa tiketi ya CHADEMA, Bernard Mwakyembe, ametoa sababu 10 zilizomfanya aondoke Chadema na kuhamia CCM. Anaripoti Gerva Lyenda … (endelea).

Mwakyembe alizitaja sababu hizo mbele ya Waandishi wa habari leo Jumamosi tarehe 29 Septemba kwenye mkutano na vyombo vya habari alioufanya jijini Dar es Salaam.

Mwakyembe alizitaja sababu hizo kuwa ni kasi ya kufanya maendeleo inayofanywa na Serikali, agenda za Chadema kutekelezwa na Serikali, kujengwa miundombinu, ujenzi wa mradi wa Stigler’s Gorge, reli ya standard gauge na kushughulika na mafisadi kunakofanywa na Serikali.

Alizitaja sababu nyingine kuwa ni kuondolewa watumishi hewa makazini, ununuzi wa ndege, kupunguza matumizi ya Serikali na kuboresha huduma za hospitali ya Muhimbili ambapo sasa watu hawaendi nje ya nchi kutafuta matibabu bora.

Mwanasiasa huyo anayedai kuwa alikuwa msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alijiunga na CCM Septemba 15 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!