Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwakyembe atoa sababu 10 za kuhamia CCM
Habari za Siasa

Mwakyembe atoa sababu 10 za kuhamia CCM

Spread the love

ALIYEKUWA Diwani wa Mtoni kwa tiketi ya CHADEMA, Bernard Mwakyembe, ametoa sababu 10 zilizomfanya aondoke Chadema na kuhamia CCM. Anaripoti Gerva Lyenda … (endelea).

Mwakyembe alizitaja sababu hizo mbele ya Waandishi wa habari leo Jumamosi tarehe 29 Septemba kwenye mkutano na vyombo vya habari alioufanya jijini Dar es Salaam.

Mwakyembe alizitaja sababu hizo kuwa ni kasi ya kufanya maendeleo inayofanywa na Serikali, agenda za Chadema kutekelezwa na Serikali, kujengwa miundombinu, ujenzi wa mradi wa Stigler’s Gorge, reli ya standard gauge na kushughulika na mafisadi kunakofanywa na Serikali.

Alizitaja sababu nyingine kuwa ni kuondolewa watumishi hewa makazini, ununuzi wa ndege, kupunguza matumizi ya Serikali na kuboresha huduma za hospitali ya Muhimbili ambapo sasa watu hawaendi nje ya nchi kutafuta matibabu bora.

Mwanasiasa huyo anayedai kuwa alikuwa msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alijiunga na CCM Septemba 15 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!