Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mrithi wa Nassar akabidhiwa jimbo
Habari za Siasa

Mrithi wa Nassar akabidhiwa jimbo

Dk. John Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki
Spread the love

MRITHI wa Joshua Nassari katika Jimbo la Arumeru Mashariki, Dk. John Pallangyo, ameapishwa leo tarehe 22 Mei 2019 kuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Job Ndugai, Spika wa Bunge amemwapisha Dk. Pallangyo, kabla ya kuapishwa kwake, alisindikizwa kwa mbwembwe na wabunge wa CCM huku wakiimba nyimbo za chama hicho.

Baada ya kula kiapo, mbunge huyo alianza kusalimia baadhi ya wabunge ambapo alianza na Kasim Majaliwa, Waziri Mkuu na wabunge wengine wa CCM,

Baada ya hapo, alikwenda upande wa upinzani na kumsalimia na kuteta kidogo na John Mnyika, Mbunge wa Kibamba na Joseph Selasin, Mbunge wa Rombo.

Dk. Pallangyo amekuwa mbunge bila kupigiwa kura. Ni baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwaengua wagombea wa vyama vingine kwa madai ya kutokuwa na sifa.

Nassari alig’olewa kwenye nafasi hiyo baada ya Spika Ndugai, kumsimamisha kutokana na kutohudhuria mikutano mitatu ya Bunge mfululizo bila kutoa taarifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!