Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko ASAS wagawa maziwa kwa Wabunge kuhamasisha unywaji
Habari Mchanganyiko

ASAS wagawa maziwa kwa Wabunge kuhamasisha unywaji

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega (kulia) akipokea maziwa aina ya Asas Dairies Milk kutoka kwa Mshauri wa Kampuni hiyo, Abdul Ally
Spread the love

WATANZANIA wamehamasishwa kutumia maziwa kwa wingi ili kuweza kutunza afya zao kutokana na kuwa maziwa hayo yanapaikana. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Wito huo umetolewa na Mshauri wa Kampuni ya Asas Dairies Milk, Abdul Ally wakati akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega pamoja na baadhi ya wabunge akiwemo mbunge wa Viti Maalum, Mariam Ditopile (CCM). 

Akizungumza kuhusu matumizi ya maziwa alisema kuwa kampuni hiyo imekuwa ikizalisha maziwa ambayo kimsingi yameboreshwa sambamba na kusambaa katika nchi nzima.

Amesema kuwa kwa sasa kampuni hiyo imekuwa ikifanya kampeni ya kusambaza maziwa hayo katika taasisi mbalimbali ikiwa pamoja na kusambaza katika shule za msingi na sekondari.

Naye mwakilishi wa Kampuni hiyo mkoa wa Dodoma, Lupyana Chagula, alisema kampuni hiyo imeona ni vema kupeleka maziwa bungeni ili kuhamasisha unywaji wa maziwa sambamba na kuchochea matumizi ya mazao ya maziwa ambayo ni bidhaa za ndani badala ya kusubiri bidhaa hiyo kutoka nje.

Kwa upande wake, Waziri Ulega alisema kampuni hiyo imekuwa ikijitahidi kuhamasisha unywaji wa maziwa na yamekuwa yakipendwa na wanywaji na kusababisha kuongeza hamasa ya unywaji wa maziwa kwa jamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

error: Content is protected !!