Friday , 9 June 2023
Home Habari Mchanganyiko ASAS wagawa maziwa kwa Wabunge kuhamasisha unywaji
Habari Mchanganyiko

ASAS wagawa maziwa kwa Wabunge kuhamasisha unywaji

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega (kulia) akipokea maziwa aina ya Asas Dairies Milk kutoka kwa Mshauri wa Kampuni hiyo, Abdul Ally
Spread the love

WATANZANIA wamehamasishwa kutumia maziwa kwa wingi ili kuweza kutunza afya zao kutokana na kuwa maziwa hayo yanapaikana. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Wito huo umetolewa na Mshauri wa Kampuni ya Asas Dairies Milk, Abdul Ally wakati akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega pamoja na baadhi ya wabunge akiwemo mbunge wa Viti Maalum, Mariam Ditopile (CCM). 

Akizungumza kuhusu matumizi ya maziwa alisema kuwa kampuni hiyo imekuwa ikizalisha maziwa ambayo kimsingi yameboreshwa sambamba na kusambaa katika nchi nzima.

Amesema kuwa kwa sasa kampuni hiyo imekuwa ikifanya kampeni ya kusambaza maziwa hayo katika taasisi mbalimbali ikiwa pamoja na kusambaza katika shule za msingi na sekondari.

Naye mwakilishi wa Kampuni hiyo mkoa wa Dodoma, Lupyana Chagula, alisema kampuni hiyo imeona ni vema kupeleka maziwa bungeni ili kuhamasisha unywaji wa maziwa sambamba na kuchochea matumizi ya mazao ya maziwa ambayo ni bidhaa za ndani badala ya kusubiri bidhaa hiyo kutoka nje.

Kwa upande wake, Waziri Ulega alisema kampuni hiyo imekuwa ikijitahidi kuhamasisha unywaji wa maziwa na yamekuwa yakipendwa na wanywaji na kusababisha kuongeza hamasa ya unywaji wa maziwa kwa jamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!