Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mnyika: Nilisema sitagombea, nijenge chama
Habari za SiasaTangulizi

Mnyika: Nilisema sitagombea, nijenge chama

Spread the love

JOHN Mnyika, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania, ametaja sababu zilizomsukuma kutogombea Ubunge wa Jimbo la Kibamba, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Mnyika ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Kibamba anayemaliza muda wake (2015 hadi 2020) , amekuwa mbunge katika vipindi viwiili mfululizo, ambapo kipindi cha kwanza alikuwa Mbunge wa Ubungo mwaka 2010 hadi 2015.

Katika kura za maoni za jimbo hilo zilizofanyika jana Jumanne, Mnyika hakuwa sehemu ya waliotia nia kwa kuchukua fomu na kurejea. Ernest Mgawe, ndiye alishika kwa kupa kura 30 kati ya 71 za wajumbe wa mkutano mkuu wa jimbo.

Wengine waliofuata nyuma ya Mgawe, ni Nemes Tarimo aliyepata kura 22 na Humphrey Sambo, ambaye alikuwa diwani wa Mbezi, aliyeambulia kura 19.

Soma zaidi hapa

John Mnyika akimbia ubunge Kibamba

Kupitia akaunti yake ya Twitter, Mnyika amezungumzia hatua yay eye kukaa kando kwenye mbio za kuwania ubunge katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020.

Katibu Mkuu huyo wa Chadema amesema, hata Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere alijiuzulu Uwaziri Mkuu wa Serikali ya Tanganyika, kwa ajili ya kukijenga Chama cha TANU.

Hata hivyo, Mnyika amesema uamuzi wa kutogombea tena aliutoa kabla ya kuteuliwa na Mkutano Mkuu wa Chadema kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Desemba mwaka 2019.

“Haya nilisema kabla ya kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu mwezi Desemba 2019, Nyerere aliwahi kuachia Uwaziri Mkuu akabaki kuimarisha TANU, nami sitagombea Ubunge 2020 nitumikie ipasavyo ukatibu mkuu wa Chadema.

Tushinde chaguzi tulete mabadiliko,” ameandika Mnyika katika ukurasa wake wa Twitter.

Kabla ya kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, tarehe 19 Desemba 2019 mbele ya wajumbe wa mkutano mkuu wa Chadema, Mnyika alisema anauweka rehani ubunge wake, ili aongeze nguvu katika mapambano ya kuitoa Serikali ya CCM madarakani.

“Nikiwa naenda jimboni kamati tendaji wananiambia tunakusikia uko huko na huko na nilikuwa nawaambia viongozi wenzangu na wananchi kwenye mikutano, tulishinda ubunge mara mbili na halmashauri, kwa muundo wa katiba mbovu inayoongoza nchi yetu, madaraka makubwa ya nchi yamewekwa mikononi mwa rais,” alisema Mnyika

“Kulikuwa na tatizo kwenye urais kunakuwa na tatizo kwenye bunge, matokeo yake hata ukiwa na madiwani wachache huwezi kufanya mabadiliko ya kutosha na suluhusisho pekee ni kuiondoa serikali na kuweka sera mpya,” alisema

Mnyika alisema, “nikawaambia nyakati zote wenzetu wa Kibamba kwa kazi ya kuiondoa CCM madarakani afadhali niweke rehani ubunge wa jimbo moja kwa manufaa ya kuletea maendeleo Watanzania kwa kuitoa serikali ya CCM madarakani.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!