Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mnyika atoa siri ya watu kupoteza imani na uchaguzi
Habari za Siasa

Mnyika atoa siri ya watu kupoteza imani na uchaguzi

John Mnyika
Spread the love

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika amesema kupungua kwa idadi ya wapiga kura katika uchaguzi kumetokana na watu kupoteza imani na mifumo ya uchaguzi. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Mnyika ameyasema hayo leo tarehe 11 Machi 2024, jijini Dar es Salaam katika Mkutano wa wadau wa siasa ulioratibiwa na Kituo cha Demokrasia nchini (TCD).

“Sisi kwa tathmini yetu tunaona idadi ya wapiga kura inapungua kwa sababu watu wamepoteza imani na mifumo ya uchaguzi” amesema Mnyika.

Mnyika amesema serikali ingeweza kuirejesha imani kwa Watanzania kwa kupeleka miswada mizuri ya mabadiliko ya sheria za vya vyama vya siasa.

“Kupelekwa miswada bungeni kungeweza kujenga imani lakini bahati mbaya kumepelekwa miswada mibovu pia karibu na uchaguzi wa serikali za mitaa” amesema Mnyika.

Amesema kuwa ili watu wawe na imani na idadi ya wapiga kura iongozeke.

“Tukitaka kuongeza idadi ya wapiga kura lazima tuongeze imani katika mifumo ya uchaguzi, lazima tudai Katiba mpya, marekebisho ya kisheria, tutengeneze uwanja sawa wa uchaguzi” amesema Mnyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!