Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Jenista Mhagama amewataka wananchi kupuuza taarifa iliyosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii kudai kuwa kutatokea Tsunami. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Kauli hiyo ya Mhagama imekuja saa chache baada ya taarifa hiyo iliyokuwa na kichwa cha habari ‘Tahadhari ya Tsunami inayoweza kusababishwa na mlipuko wa Volcano’ kuwa itaathiri maeneo ya mwambo wa Pwani.
Akizungumza na Kituo cha Runinga cha Azam leo Jumatano usiku, Mhagama amesema watalaam wa masuala ya hali ya hewa wanaaendelea na mikakati mbalimbali ya kukabiliana na mvua za elnino.
Amesema taarifa hiyo kuhusu Tsunami sio taarifa rasmi na Ofisi ya Waziri mkuu imewasiliana na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania na kudhibitisha hakuna Tsunami.
Leave a comment