Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya Ubungo: Magufuli ameingizwa chaka
Habari za SiasaTangulizi

Meya Ubungo: Magufuli ameingizwa chaka

Rais John Magufuli
Spread the love

WALIO MPOTOSHA MH. RAIS KUHUSU MAPATO YA HALMASHAURI ZA MKOA WA DAR ES SALAAM WA WAJIBISHWE

Tangu jana nimepigiwa simu na Waandishi wa habari na wadau wa Maendeleo katika Halmashauri za jiji la Dar es salaam kutaka nitoe ufafanuzi juu ya Mapato ya Jiji la Dar es salaam kupitwa na Jiji jipya la Dodoma.

Ukweli ni kwamba Jiji la Dar es salaam haliwezi kamwe kupitwa Mapato yake na Jiji la Dodoma.

pana utofauti wa Kimuundo wa Jiji la Dar es salaam lenye watu Millioni 5 na Jiji la Dodoma lenye watu Millioni 2

Dar es salaam,Halmashauri ya jiji ni moja wapo katika Halmashauri 6( Kigamboni,Temeke,Ubungo,Kinondoni,Ilala DSM city council lenyewe) kwa Mkoa wa Dar es salaam,wakati Dodoma wao wana Halmashauri moja tuh ya Jiji la Dodoma lenye watu Millioni 2.

Mtu akitaka kulinganisha ulipaji wa mapato kataka Majiji haya ni kama ifuatavyo.

1.Halamashauri ya Manispaa ya Ilala
Budget ya 2017/18 Walipanga makusanyo 46,621 718 036 walichokusanya 44,505,251,223, makusanyo yatakuwa asilimia 95.5

2.Halamshauri ya Manispaa ya Kinondoni
Budget review 2017/2018 Makadirio mapato ya ndani yalikuwa ni Billioni 31,619,825,405.08 na Wamekusanya Billioni 29,754,382,564.86 sawa na Asilimia 94.

3.Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo
Makadirio ya Budget Mapato ya ndani ni 16,505,598,500.00 wakati wamekusanya 13,496,386,027.00 sawa na asilimia 81.8

4. Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam
Makadirio ya Mapato ya ndani kwa Mwaka wa 2017/2018 yalikuwa ni billion 16,413,537 000.00 na wamekusanya 16, 849,660,891.44 sawa na asilimia 102

5. Halmashauri ya Manispaa ya Temeke
Bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 Mapato ya ndani
walipanga kukusanya Billioni 30,910,528,600 wamepata billioni 29,034,531,092 sawa na asilimia 94.

6. Halamshauri ya manispaa ya Kigamboni
Bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 Mapato ya ndani ni Bajeti kigamboni ni Billioni 9,218,868,000 makusanyo harisi ni Billioni 5,478,544,722 sawa asilimia 59

SASA UKITAKA KULINGANISHA
chukua mapato ya Halamshauri zote za Dar es salaam ambapo jumla walioanga kukusanya Billioni 151,290,075,441 na wakafanikiwa kukusanya kiasi cha Billioni 139,118,756,519,90 sawa na Asilimia 91.95

kiasi hiki cha fedha ndicho kimechangiwa na watu Millioni 5 wa Dar es salaam sasa ndipo Ulinganishe na Mapato yote ya Jiji la Dodoma waliopata Billioni 24.4 kwa makusanyo ya watu Millioni 2.

Swali Je Billioni 139.118,756,519.90 ni ndogo kuliko Billioni 24.4

Mwisho
Nikubaliane na Mheshimiwa Rais kuwa kuna Upigaji wa Mapato kwenye Halmashauri wa kufa Mtu! hilo halina Ubishi hata kidogo, Waziri Jaffo anajua tunavyopambana kuzuia Mianya hiyo.
Na pili ni utaratibu huu Mzuri wa Mheshimiwa Rais wa kilinganisha na Kushindanisha Mapato ya Halmashauri mbalimbali Nchi nzima,Utaratibu huu Unafanya tupambane kuwa Vinara wa Ukusanyaji Mapato.
Lakini pia Nichukue nafasi kuwapongeza Dodoma na Ubungo halmashauri mpyaa kufanya vizuri kwa mara ya kwanza.

IMETOLEWA Na

Boniface Jacob
MSTAHIKI MEYA
MANISPAA YA UBUNGO

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!