Friday , 2 June 2023
Home Kitengo Michezo Yanga kumuaga rasmi Canavaro Agosti 12
Michezo

Yanga kumuaga rasmi Canavaro Agosti 12

Spread the love

ALIYEKUWA nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ”Cannavaro” anatarajiwa kuagwa rasmi ndani ya klabu hiyo tarehe 12 Agosti, 2018 kwa mchezo maalumu wa kirafiki baada ya kutangaza kutundika daruga. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Katika taarifa rasmi iliyotolewa na uongozi wa klabu hiyo kupitia kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii, imesema klabu hiyo inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki na timu ambayo bado haijafaamika kwa lengo la kumuaga nahodha huyo.

Cannavaro ambaye alitangaza kustaafu soka 26 Juni, mwaka huu, amefanikiwa kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka 12, toka alipojiunga nayo Mwaka 2006 akitokea Malindi FC, inayoshiriki Ligi Kuu Zanzibar.

Yanga ambayo kwa sasa imeweka kambi mkoani Morogoro kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu pamoja na mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger unaotarajia kuchezwa 19 Agosti, 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Dk. Mkwizu: Afrika tudumishe utamaduni

Spread the love  MWENYEKITI wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Mkoa wa...

Michezo

‘EONII’ kuteka tasnia ya filamu

Spread the love  UZINDUZI wa Filamu ya Kisayansi ya ‘EONII’ uliofanyika Mei...

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

error: Content is protected !!