Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga kumuaga rasmi Canavaro Agosti 12
Michezo

Yanga kumuaga rasmi Canavaro Agosti 12

Spread the love

ALIYEKUWA nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ”Cannavaro” anatarajiwa kuagwa rasmi ndani ya klabu hiyo tarehe 12 Agosti, 2018 kwa mchezo maalumu wa kirafiki baada ya kutangaza kutundika daruga. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Katika taarifa rasmi iliyotolewa na uongozi wa klabu hiyo kupitia kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii, imesema klabu hiyo inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki na timu ambayo bado haijafaamika kwa lengo la kumuaga nahodha huyo.

Cannavaro ambaye alitangaza kustaafu soka 26 Juni, mwaka huu, amefanikiwa kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka 12, toka alipojiunga nayo Mwaka 2006 akitokea Malindi FC, inayoshiriki Ligi Kuu Zanzibar.

Yanga ambayo kwa sasa imeweka kambi mkoani Morogoro kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu pamoja na mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger unaotarajia kuchezwa 19 Agosti, 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!