Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya Moshi akanusha madai kupigwa na diwani, vita ya kisiasa yatajwa
Habari za Siasa

Meya Moshi akanusha madai kupigwa na diwani, vita ya kisiasa yatajwa

Meya wa Manispaa ya Moshi, Zuberi Kidumo
Spread the love

 

MEYA wa Manispaa ya Moshi, Zuberi Kidumo amekanusha madai ya kupigwa na Diwani wa kata ya Mji Mpya – Moshi, Abuu Shayo (CCM) katika Kikao cha kamati ya mipango miji na ardhi katika manispaa hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Taarifa za kupigwa kwa Meya huyo ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Njoro, zimesambaa jana Alhamisi katika mitandao ya kijamii, zikidai kuwa alishushiwa kipigo baada ya ‘kumkwida’ Diwani Shayo aliyehoji ubadhirifu katika halmashauri hiyo.

Aidha, akizungumza leo tarehe 14 Julai 2023 na waandishi wa habari wilayani Hai, Meya Kidumo ameeleza kushangazwa na taarifa hizo baada ya kuziona kwenye mitandao ya kijamii.

Amefafanua kuwa ni kweli kulikuwa na kikao cha Kamati ya Mipango miji na Ardhi katika manispaa hiyo kilichofanyika jana saa nne hadi saa saba.
“Baada kikao kuisha watu walipata chakula na mimi nilienda kwenye kikao cha halmashauri kuu ya kata Njoro ambayo nini ni diwani wake.

“Nilipotoka Njoro nikaelekea uwanja ambako kulikuwa na mechi lakini cha ajabu ndipo nikaona hizo taarifa,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

error: Content is protected !!