Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee ageukwa, Spika Ndugai ‘aokoa’ jahazi
Habari za Siasa

Mdee ageukwa, Spika Ndugai ‘aokoa’ jahazi

Halima Mdee, Mbunge wa Chadema Viti Maalim
Spread the love

 

WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ama wamemchoka Halima Mdee, mbunge asiye na chama bungeni au wamekerwa na kauli yake, aliyosema ‘kuna wabunge njuka.’ Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mdee alitumia neno wabunge njuka akimaanisha wabunge wapya ndani ya Bunge.

Wabunge hao wameeleza kukera na kauli ya Mdee ambaye tarehe 27 Novemba 2020, yeye na wenzake 18, walifukuzwa Chadema wakituhumiwa kwa usaliti kwa kujipeleka bungeni kuapishwa.

“Ombi langu kwa sisi tuliopewa dhamana na wananchi wa Tanzania, bila kujali vyama vyetu, bila kujali umeingilia mlango gani maana wapo wabunge hapa vyama vyao vimewakana,” amesema Jerry Silaa, Mbunge wa Ukonga, alipokuwa akichangia mpango wa maendeleo wa miaka mitano 2021-2026.

Silaa amesema, “…msemaji hapa anasema ndege zimepaki, ndege haziruki kama kunguru. Tumenunua ndege Q400 za safari za ndani na Air Bus masafa marefu.”

Jerry Silaa

Huku wabunge wakishangilia na Silaa akitaka kuendelea kudadavua, Spika Job Ndugai ‘aliingilia’ kati kwa kumshukuru Silaa kwa mchango wake.

Hata hivyo, Silaa alitaka kuendelea lakini Spika Ndugai akarejea tena maneno yale yale ya kumshukuru ‘asante sana,’ kwa maana ya kutaka Silaa akae chini.

Kauli ya Silaa ilipongezwa kwa idadi kubwa na wabunge wa CCM, ambao ndio waliwapongeza Mdee na kundi lake wakati walipoingia bungeni kwa mara ya kwanza.

Spika Ndugai akasemama na kusema “hilo ndiyo bungeni bwana, naona njuka wamechachamaa, wamekataa kabisa kuitwa njuka, Halima umechokoza mwenyewe, ndiyo raha ya mjengoni.”

“Mjadala ya moto kabisa na mwisho wa siku tutafika tu,” amesema Ndugai

Mdee alipata ‘shambulizi’ linguine kutoka kwa Godwin Kunambi, Mbunge wa Mlimba (CCM). Akikamilisha mchango wake alimuonya Mdee, aliyewahi kuwa mbunge wa Kawe.

Job Ndugai Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania

“Kwanza nianze na lugha za kejeli, lugha za kuudhi na sisi wengine ni vijana pia, bado hata umri wa busara haujafika…., namuonya aache lugha za kejeli humu ndani ya bunge. Namuaonya tu, hamna njuka hapa, njuka maana yake nini?” amesema Kunambi huku wabunge wa CCM wakimshangilia.

“Amezungumzia suala la ATCL, ni huduma tu, anakuja hapa anatudanganya, tunampigia makofu tu,” amesema Kunambi

Baada ya Kunambi kumaliza kuzungumza,mmoja aliwasha kipaza sauti na kusema ‘taarifa, taarifa mheshimiwa spika, taarifa,” hata hivyo, Spika Ndugai alipuuza na kisha kusema “jamani tusikilizane, bahati nzuri hakuna taarifa, kwa hiyo tunaendelea.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!