Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Aswaar waanza kufunga Ramadhani
Habari Mchanganyiko

Aswaar waanza kufunga Ramadhani

Spread the love

 

WAISLAM wenye madhehebu ya Answaar nchini Tanzania, wameanza mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan leo tarehe 13 Aprili 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa zinaeleza, Pamoja na maeneo mengine, mwezi umeonekana Saudi Arabia, Lebanon na Misri.

“Aprili 13, 2021 itakuwa siku ya kwanza ya Mwezi Mtukufu wa Ramdhani,” ilieleza taarifa ya mamlaka ya kutangaza mwezi nchini Misri.

Katika nchini ya Lebanon, kiongozi mkuu wa madhehebu ya Sunni, Mufti Sheikh Abdellatif Deryan ametoa taarifa kwa Waislam wa nchi hiyo kuanza kufunga Ramadhani leo.

Baadhi ya Waislam katika nchi za Afrika, wenye msimamo wa kufunga kutokana na mwezi kuonekana sehemu yoyote duniani, wameanza funga hiyo leo.

Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni moja ya nguzo tano zilizojenga dini ya Kiislam. Nguzo zingine ni Kumuamini Mungu Mmoja, kusimamisha swala tano, kuhiji Makka na kutoa zaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!