Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mch. Msigwa ayamwaga bungeni aliyoyaona Segerea
Habari za SiasaTangulizi

Mch. Msigwa ayamwaga bungeni aliyoyaona Segerea

Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini akiwa chini ya ulinzi wa Polisi katika moja ya kesi zake
Spread the love

MBUNGE wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (Chadema) amedai Tanzania kwa sasa kuna msongamano mkubwa wa wafungwa ambapo amehoji Serikali inachukua hatua gani kupunguza msongamano huo. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Akiuliza swali la nyongeza jana bungeni Msigwa alidai kuwa gereza la Segerea limezidiwa na mahabausu ambapo lina uwezo wa kuchukua mahabusu 700, lakini waliopo kwa sasa ni mahabusu na wafungwa  2400.

“Ukienda katika Magereza zetu kuna msongamano mkubwa sana kwa mfano Gereza la Segerea ambalo nililipitia juzi lina uwezo wa kuchukua mahabusu 700 lakini sasa hivi lina mahabusu na wafungwa 2400.

“Wanalazimika watu kulala upande mmoja mmoja kwa zamu baada ya muda inapigwa ‘alarm’ kisha mnageukia upande mwingine huu ni ukiukwaji kabisa wa haki za binadamu na watoto wengi wapo pale chini ya umri wanatakiwa waende shule.

“Ni kwanini Serikali imekuwa ikipeleka wanasheria kutetea kesi za Serikali ambao wamekuwa wakilazimisha wale ambao wanaweza kupata dhamana waende kukaa mahabusu kama ambavyo kesi zetu zilikuwa zina dhamana lakini mawakili wa Serikali walikuwa wanalazimisha tuende kule tukaongeze msongamano,” ameuliza Msigwa.

Akijibu kwa niaba ya Serikali, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha amesema kuwekwa ndani kwa muda mrefu kwa mahabusu siyo kweli kwamba Serikali haitaki kesi hizo zimalizike haraka.

“Sababu za msingi ni sababu ya usalama wao, wakienda nje wanaweza wakapata matatizo ikiwemo Serikali kuwalinda pili kuna watuhumiwa wakitoka nje wataenda kuharibu ushahidi,” amesema

Naye, Mbunge wa Tarime Mjini Ester Matiku (Chadema) katika swali lake la nyongeza aliitaka serikali iwaachie kina mama ambao wamefungwa huku wakiwa wanaumwa.

“Nimekuwa Segerea Mheshimiwa Spika kule kuna wamama wamefungwa wanadaiwa mathalani 150,000 lakini amefungwa miezi sita kwa gharama ambazo amezitoa Naibu Waziri zinavuka mpaka 200,000.

“Kwanini Serikali isitumie busara kwa kina mama ambao wengine wana watoto wachanga wanafungwa kwa kesi ya shilingi 100,000 mpaka 200,000 na Serikali inatumia gharama kubwa katika gharama za chakula,” amehoji Matiko.

Akijibu swali hilo, Ole Nasha amesema suala hilo ni la kisheria hivyo kama Mbunge anaona hoja hiyo inamashiko apeleke hoja binafsi bungeni.

Akiongezea majibu, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba, alisema hawawezi kuwaacha wahalifu nje kutokana na kuogopa Magereza kujaa.

“Niweke kumbukumbu sawa sio kila Magereza yana msongamano tuna baadhi ya Magereza katika mikoa ile ambayo kiwango cha uhalifu ni mdogo mfano Lindi na kule Mlalo,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!