Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Mfungwa mmoja kutumia laki moja kwa siku
Tangulizi

Mfungwa mmoja kutumia laki moja kwa siku

Spread the love

WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi imesema gharama za chakula kwa mfungwa mmoja kwa siku ni wastani wa shilingi 1,342. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Hayo yalielezwa leo bungeni na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamadi Masauni alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Njombe Mjini, Edward Mwalongo (CCM).

Katika swali hilo Mwalongo alitaka kujua Serikali inatumia kiasi cha shilingi ngapi kuhudumia mfungwa mmoja kwa siku kwa ajili ya chakula.

 “Vitendo kama kulala chini, kulala bila blanketi au shuka vimekuwa vya kawaida kabisa katika Magereza yetu. Je hii nayo ni sehemu ya adhabu ambayo wafungwa wanapewa kwa mujibu wa sheria,” alihoji Mbunge huyo.

Akijibu, Masauni amesema Jeshi la Magereza katika kutekeleza majukumu yake pia hutoa huduma ya chakula kwa wahalifu kupitia bajeti iliyotengwa na Serikali kila mwaka wa fedha.

Naibu Waziri huyo amesema gharama za chakula kwa mfungwa mmoja kwa siku ni wastani wa shilingi 1,342.

Amesema Serikali imeendelea kuboresha huduma za wafungwa na mahabusu kwa kununua vifaa mbalimbali vya malazi ikiwemo, magodoro shuka, mablanketi na madawa ya kuua wadudu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atua Uturuki kwa ziara ya siku 5

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano amewasili nchini Uturuki kwa...

error: Content is protected !!