Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Ngorongoro aachiwa, asema harudi nyuma, ashangaa kukamatwa bila kibali cha Spika
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge Ngorongoro aachiwa, asema harudi nyuma, ashangaa kukamatwa bila kibali cha Spika

Spread the love

HATIMAYE Mbunge wa Ngorongoro, Emmanuel Ole Shangai (CCM) ambaye alidaiwa kushikiliwa na polisi tangu tarehe 21 Agosti 2023 ameachiwa huru leo huku akisisitiza kwa kuwa yupo upande wa wananchi lazima apate matatizo, na hilo halitomrudisha nyuma hata siku moja. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Mbunge huyo alidaiwa kushikiliwa na jeshi hilo, akiwa njiani kuelekea kituo cha Polisi wilayani Karatu, kutokana na tuhuma za kuhusishwa kupanga tukio la kushambuliwa waandishi wa habari.

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 23 Agosti 2023 Mbunge huyo amesema  amesita kutaja tuhuma alizokutwa nazo na kufafanua kuwa zitajulikana mahakama.

Bila kutaja lini atafikishwa mahakamani, Mbunge huyo wa CCM amedai kwa siku zote tatu alizokuwa ameshikiliwa na polisi hakula chochote.

“Pia nimejifunza kuwa binadamu unaweza kukaa siku tatu bila kula na hautakufa na hata ningekaa siku saba nisingekula siku saba,” amesema.

Aidha, ameeleza kushangazwa na hatua ya polisi kumkamata bila kibali cha Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson.

“Ninachoshangaa wote wanajua, polisi ndio wanasimamia sheria zetu na Bunge ndio linatunga sheria niliamini kwamba kama walikuwa wananihitaji na hicho ndio nilikuwa nasubiri wangemuandikia Spika barua alafu Spika anijulishe.

“Nakumbuka mwaka jana Aprili niliitwa kuhojiwa kuhusiana na suala la Loliondo, Spika ndio alitoa kibali cha mimi kuhojiwa nashangaa leo kwanini hawakusubiri mpaka Spika atoe barua… najua kuna presha za kisiasa na mimi ni mwanasiasa nitaendelea kuishi kwenye siasa,” amesema.

Pamoja na mambo mengine amewataka wananchi wajue yeye ni kiongozi wao hata akikamatwa mara 10 ataendelea kuwa na msimamo wao kwa sababu walimchagua kwa ajili yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!