Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge aliyetishia kuhamia CCM, ahamia kweli
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge aliyetishia kuhamia CCM, ahamia kweli

Spread the love

MBUNGE wa Serengeti (Chadema), Marwa Chacha amejiuzulu uanachama wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza leo Septemba 27, 2018 Chacha amesema amechukua uamuzi huo kumuunga mkono mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli.

Amesema wakati akigombea ubunge aliahidi kuwaletea maendeleo wananchi wake lakini dhamira yake haijafanikiwa kutoka na vikwazo anavyokumbana navyo ndani ya Chadema.

Chacha amewataka wakazi wa Serengeti kumchagua mtu atakayeweza kushirikiana nao pamoja ili kuleta maendeleo kupitia CCM.

Mbunge huyo alikutana na wakati mgumu wakati wa ziara ya Rais Magufuli mkoani Mara ya kuzomewa na wananchi alipobanwa na maswali.

Baada ya kuzomewa Chacha alipopata nafasi kuzungumza alisema, wanamzomea kwa sababu yeye siye CCM lakini ipo siku naye atakuwa CCM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia apangua mawaziri

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la...

Habari za Siasa

RC mstaafu afariki dunia, CCM yamlilia

Spread the loveALIYEWAHI kuwa mkuu wa mikoa ya Dodoma, Mara, Mtwara na...

Habari za Siasa

Marekani kuwekeza Dola 500 Mil kupeleka bidhaa na huduma Tanzania

Spread the loveMAKAMU wa Rais wa Marekani, Kamala Harris amesema miongoni mwa...

Habari za Siasa

Kamala ataja hatua mpya kuimarisha uhusiano wa kibiashara Tanzania, Marekani

Spread the loveKATIKA kuimaridha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi baina ya Tanzania...

error: Content is protected !!