Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Viongozi wa vijiji wasakwa na Jeshi la Polisi, kisa bangi
Habari Mchanganyiko

Viongozi wa vijiji wasakwa na Jeshi la Polisi, kisa bangi

Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Arusha linawasaka viongozi wa kijiji cha Kisimiri Juu kilichopo wilayani Arumeru kwa tuhuma za kukiuka agizo la serikali pamoja na kukwamisha msako wa bhangi kijijini hapo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hayo yalisemwa jana tarehe 27 Septemba 2018 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng’azi wakati kizungumza na Wanahabari mkoani humo.

Kamanda Ng’azi alisema kuwa, viongozi hao walifunga ofisi huku wanakijiji wakijificha wakati wa msako uliofanyika alfajiri ya jana baada ya Jeshi la Polisi kudokezwa kuhusu usafirishaji wa bangi uliopangwa kufanyika jana.

“Tunaendelea kuwatafuta viongozi wa kamati za ulinzi na usalama na wa kijiji, kwa ajili ya kuwachukulia hatua za kisheria kwa kuwa wana wajibu wa kuhakikisha katika eneo lao hakuna biashara ya dawa za kulevya inayofanyika.

“Viongozi hao wamekiuka agizo la serikali linalomtaka kila kiongozi katika eneo lake ahakikishe kwamba halilimwi bhangi,” alisema Kamanda Ng’azi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!