Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ahoji vitisho vya polisi
Habari za Siasa

Mbunge ahoji vitisho vya polisi

Devotha Minja, Mbunge wa Viti Maalum Chadema
Spread the love

DEVOTHA Minja, Mbunge wa Viti Maalum mkoani Morogoro (Chadema), ameeleza kukerwa na kauli za vitisho zinazotolewa na Jeshi la Polisi nchini. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Amehoji sababu za polisi kujenga utamaduni wa kutoa vitisho kwa wananchi ambapo ndio wanaolipa kodi inayotumika kuwapa mishahara.

Mbunge huyo ameuliza swali leo tarehe 9 Aprili 2019 bungeni jijini Dodoma, akiitaka Wizara ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI kutoa tamko kuhusu kauli iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa iliyolenga kuonya watu waliotangaza nia ya kuandamana.

“Si wakuu wa mikoa na wilaya ambao hawafanyi vizuri, wapo pia MaRPC hawafanyi vizuri, RPC anaposema wananchi wakiandamana wanapigwa hadi wachakazwe, hivi anavyolipwa mshahara kazi ni kuchakaza wananchi?” amehoji Minja.

Akijibu swali la Minja, Waziri wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Suleiman Jaffo amesema vyombo vya dola vinaendeshwa kwa kanuni na sheria zake, hivyo serikali haiwezi kuviingilia na kuwataka wananchi kufuata sheria ili kuepuka migogoro.

“Jambo la kwanza, tuweke ushirikiano kila eneo, vyombo vingine vinaendeshwa kwa kanuni, hatuwezi kuingilia mambo yao ya ndani. Ni vyema wananchi wakafuata sheria ili kuondoa migongano,” amesema Jaffo.

Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini alihoji ukimya wa serikali kuhusu vitendo vya baadhi ya wakuu wa wilaya na mikoa wanaodaiwa kuwanyanyasa wananchi .

“Wilaya ya Hai mkuu wa wilaya bado anaendelea na vitendo vya kukamata wananchi na wawekezaji na kuwatumia maskari kushawishi wanasiasa wahame vyama vyao, sasa ningependa kujua baada ya kauli za waziri ni hatua zipi serikali imepanga kuchukua,” amehoji Selasini.

Akijibu swali la Selasini, Jaffo amesema “Ttumetoa maelekezo kwa watu wetu kwa kuwa wamepewa dhamana, kitendo hicho si sawa sawa jukumu letu sasa kuwachukulia hatua na rais ametoa maagizo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!