Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ahoji vitisho vya polisi
Habari za Siasa

Mbunge ahoji vitisho vya polisi

Devotha Minja, Mbunge wa Viti Maalum Chadema
Spread the love

DEVOTHA Minja, Mbunge wa Viti Maalum mkoani Morogoro (Chadema), ameeleza kukerwa na kauli za vitisho zinazotolewa na Jeshi la Polisi nchini. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Amehoji sababu za polisi kujenga utamaduni wa kutoa vitisho kwa wananchi ambapo ndio wanaolipa kodi inayotumika kuwapa mishahara.

Mbunge huyo ameuliza swali leo tarehe 9 Aprili 2019 bungeni jijini Dodoma, akiitaka Wizara ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI kutoa tamko kuhusu kauli iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa iliyolenga kuonya watu waliotangaza nia ya kuandamana.

“Si wakuu wa mikoa na wilaya ambao hawafanyi vizuri, wapo pia MaRPC hawafanyi vizuri, RPC anaposema wananchi wakiandamana wanapigwa hadi wachakazwe, hivi anavyolipwa mshahara kazi ni kuchakaza wananchi?” amehoji Minja.

Akijibu swali la Minja, Waziri wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Suleiman Jaffo amesema vyombo vya dola vinaendeshwa kwa kanuni na sheria zake, hivyo serikali haiwezi kuviingilia na kuwataka wananchi kufuata sheria ili kuepuka migogoro.

“Jambo la kwanza, tuweke ushirikiano kila eneo, vyombo vingine vinaendeshwa kwa kanuni, hatuwezi kuingilia mambo yao ya ndani. Ni vyema wananchi wakafuata sheria ili kuondoa migongano,” amesema Jaffo.

Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini alihoji ukimya wa serikali kuhusu vitendo vya baadhi ya wakuu wa wilaya na mikoa wanaodaiwa kuwanyanyasa wananchi .

“Wilaya ya Hai mkuu wa wilaya bado anaendelea na vitendo vya kukamata wananchi na wawekezaji na kuwatumia maskari kushawishi wanasiasa wahame vyama vyao, sasa ningependa kujua baada ya kauli za waziri ni hatua zipi serikali imepanga kuchukua,” amehoji Selasini.

Akijibu swali la Selasini, Jaffo amesema “Ttumetoa maelekezo kwa watu wetu kwa kuwa wamepewa dhamana, kitendo hicho si sawa sawa jukumu letu sasa kuwachukulia hatua na rais ametoa maagizo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

error: Content is protected !!